Language

Saturday 2 March 2013

MAHUSIANO: UNAJUA NGONO HUPUNGUZA MSONGO WA MAWAZO (STRESS)??? PIA FAIDA ZA MANII ZIKO HAPA.

UTAFITI uliofanywa na Chuo Kikuu cha State cha jijini New York nchini Marekani unaeleza kuwa manii ni nzuri kwa wanawake kwani huwaondolea msongo wa mawazo.


Pia, watafiti hao wamesema wanawake wanaofanya tendo la ndoa mara kwa mara bila kutumia kinga (mapenzi salama) wanakuwa na kiwango kidogo cha msongo wa mawazo na hufanya vizuri katika vipimo vya akili.

Hali hii wamesema wataalam hao kuwa inatokana na manii kuwa na kemikali ambazo humfanya mtu kuwa vizuri kihisia, huongeza upendo/unyenyekevu, huchochea mtu kupata usingizi na huwa na angalau aina tatu za kemikali za kuondoa msongo wa mawazo (anti-depressants).

Utafiti huo uliofanywa kwa kuwahoji wanawake 293 kwa kufuatilia maisha yao ya kujamiana dhidi ya afya za akili zao. Manii huwa na mchanganyiko wa kemikali aina ya cortisol ambayo huongeza upendo, kemikali aina ya esterone na oxytocin ambazo zote humfanya mtu kuwa vizuri  kihisia.


Pia, huwa na homoni aina za ‘thyrotropin releasing hormone’, ambayo huondoa msongo wa mawazo, melatonin ambayo huchochea usingizi na serotonin ambayo ni homoni inayoondoa msongo wa mawazo.

Kutokana kuwapo kwa mchanganyiko wa kemikali na homoni hizo kwenye manii

Matokeo ya utafiti
Matokeo muhimu ya utafiti huu ambao umechapishwa katika jarida la ‘Archives of Sexual Behaviour’ ni kwamba hata baada ya baadhi ya watafitiwa kuongeza kiwango chao cha kujamiana, wale ambao walikuwa hawatumii kinga yoyote walikuwa na kiwango kidogo cha msongo wa mawazo tofauti na wale ambao walikuwa wakitumia kinga kama kondomu wakati wa kujamiana.


No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...