Language

Sunday 13 January 2013

HABARI: WANNE WAFA SOMALIA


Wakaazi wa mji mmoja wa kusini mwa Somalia wanasema raia wanane waliuwawa katika jaribio lilofanywa na makamando wa Ufaransa kumkomboa mwananchi mwenzao aliyezuwiliwa na wapiganaji. 

Ramani ya mji wa Bulo Marer

Wengine walikufa katika mapambano ya risasi.
Mwanajeshi mmoja wa Ufaransa alikufa Jumamosi kwenye operesheni hiyo na mwengine ametoweka.
Wapiganaji wa Kiislamu wa Al Shabaab ambao walikuwa wanamzuwia askari wa ujasusi wa Ufaransa walisema afisa huyo yuhai, lakini Ufaransa inasema pengine aliuwawa.

HABARI: MAJESHI YA MALI YAWASHINDA WAASI

Majeshi ya Mali yamewafurusha waasi wa Kiislamu kutoka mji muhimu katika eneo la kati nchini humo,baada ya Ufaransa kuingilia kati jana Ijumaa(11.01.2013)kwa mashambulio ya anga na kuzuwia waasi hao kusonga mbele.
 
Bewaffnete Tuareg-Kämpfer auf ihrem Pick-up; Nordmali am 15.02.2012. Nach dem Sturz von Gaddafi in Libyen ist der Bürgerkrieg in Mali zwischen Tuareg-Rebellen und den Regierungstruppen eskaliert. Fast 130.000 Menschen befinden sich laut UN auf der Flucht. Rund die Hälfte flüchtete ins Ausland, die andere Hälfte sind Binnenflüchtlinge. Durch die bestehende Nahrungsmittelknappheit in der Sahelzone droht eine humanitäre Katastrophe.
Waasi wa nchi hiyo wanadhibiti eneo la kaskazini hadi sasa.
Serikali za mataifa ya magharibi , hususan mkoloni wa zamani wa nchi hiyo ufaransa , imeeleza hali ya tahadhari baada ya muungano wa waasi hao wenye mafungamano na kundi la al-Qaeda kuukamata mji wa Konna siku ya Alhamis (10.01.2013), ikiwa ni njia ya kuingilia katika mji mkuu Bamako, kilometa 600 kusini mwa nchi hiyo.

BURUDANI: MISTARI YA DEAR GOD (LYRICS) YA KALA JEREMIAH

Dear God by Kala Jeremiah

Intro:
Rock town records
Dear God let me to talk you
cause am in jungle God
I need your help
I watch my back
I see myself!!


Verse:
Asante Mungu leo ni siku nyingine
nakuja mbele yako baba nina ombi jingine
Baba wewe ndo kimbilio sina tena mwingine
si unacheki sina furaha kama watu wengine
Wengine wanakula bata na kusaza zingine
mimi bado niko ziro na masela wengine
Pengine labda umesisahau au umenichoka pengine
lakini hapana we sio kama viumbe wengine
Uliniumba wewe baba sio mtu mwingine
tena mimba yangu ililelewa na baba mwingine
Baba alikua busy na mademu wengine
nimeshamsamehe mwambie ana mtoto mwingine
Mwambie nampenda sana sina baba mwingine
mwisho wayote mlaze pema kama watu wengine
Tukiachana na hayo nina mambo mengine
baba mziki wangu ndio tatizo kubwa jingine
Nachana sana promo wanapewa wengine
wengine wanasema niende kwa mganga pengine
Lakini mi nimebatizwa kama wakristo wengine
naijua Biblia zaidi ya vitabu vingine
Mungu wa islael Mungu wa mataifa mengine
Mungu wa Yakobo Mungu wa Isaka Mungu watu wengine
Usikie kuomba kwangu unipe njia nyingine
Naombea watoto mayatima na wenye shida wengine
Wananchi maskini na tabaka jingine
Mungu baba tupe neema kama nchi zingine
Watembelee mafisadi mmoja baada ya mwingine 
wakumbushe kula kwa jasho kama watu wengine
Ona mpaka nasahau mengine
baba ajira zipo chache hawapati wengine
Vijana wanakula unga hawana kazi nyingine 
dada zetu wanajiuza wengine
Pengine labda ndio sodoma na gomora nyingine 
wanaume sikuhizi ni mashoga wengine
Wanadai haki zao kama haki zingine
wanaandamana hadharani mataifa mengine
Wanaoana kwa harusi kama ndoa zingine
tuachane na hayo masuala nina swala jingine
Hivi ni kweli umewatuma manabii wengine
maana kila kukicha kuna kanisa jingine
Huyu nabii na huyu ni nabii mwingine
huyu anaponda na huyu anampinga mwingine
Wanahubiri kuhusu pesa sio kitu kingine
toa ndugu toa toa ulichonacho kingine
Mungu nionyeshe njia nioneshe ishara nyingine 
yapo mambo mengi tu siwezi taja mengine
Hata demu wangu nahisi ana mshikaji mwingine 
mana kabadilika kawa kama yule mwingine
Niliyemfuma live akiwa na boya mwingine
nisamehe dhambi ya kuzini sina dhambi nyingine
Mwokozi wangu niongeze pesa zingine
rafiki zangu niongeze tena wengine
Wawe wote waukweli sio masnitch wengine
wakuchukua siri na kuvujisha kwingine
Naombea madaktari waongezwe posho zingine 
ili usije kutokea mgomo tena mwingine
Mana walikufa watu wasije wakafa wengine
mwisho wa yote nashukuru kwa uhai mwingine
Ninajua sahizi watu wamelazwa wengine
rafiki zangu walishagongwa na magari wengine
Kama Farook Warango na machizi wengine 
mlaze pema Kanumba na rafiki wengine
Tutaonana Yesu akirudi kwa mara nyingine 
asante sana kwa baraza jingine
Japo magamba yamevuka yakabaki mengine
classic moja ina watu wengine
Wanadai nchi imeuzwa kwa jamaa mwingine 
Sajuki Vengu na wagonjwa wengine
Wanyooshee mkono wako wape Afya nyingine
Ameen!!

BURUDANI: HII NDIO MISTARI(LYRICS) YA KESHO YA DIAMOND

Song: Kesho


{Chorous}
=i> Mi nataka kesho twende nikupeleke nyumbani
nataka kesho twende ukamuone mama x2
{Verse 1}
=I> Kwanza kabisa ntanyonga Tai
T”shirt na Jeans ntatupa kidogo..
Unite Nasibu usiniite Dai
Asije kukuona muhuni akapandisha Mbogo…
Naukifika uagize Chai
Savanna Takila uzipe kisogo…
Kuhusu mavazi kimini haifai
Tupia pendeza ila za Hekima Logo…
=I> Even though wanaponda eti we ni kicheche
Waambie ndoo chaguo langu sasa wanicheke x2
Chorous}
=I> Minataka kesho twende nikupeleke nyumbani
Nataka kesho twende ukamuone mama x2
{Verse 2}
Usilete swaga za Nainai
Ukanyoa kiduku kama Moze Iyobo..
Eti shoping twende Tai
wakati Dadaangu anaduka kigogo..
Ukikuta Nguna usikatae
we zuga unapenda hata kama wa Muhogo..
Kuhusu kabila mbona Sadai
Mama angu hana noma hata kama Mgogo
=I> Even though wanaponda eti we ni kicheche
Waambie ndoo chaguo langu sasa wanicheke x2
{Chorous}
=I> Minataka kesho twende nikupeleke nyumbani
Nataka kesho twende ukamuone mama x2
Bridge
Mama yangu mama…
Mama Naseeb mama…
Mama Diamond mama…
Mama yangu nyumbani…
Mama Chali mama…
Mama Sepetu mama…
Mama Kidoti mama…
Kwa mama Diamond nyumbani…
{Chorous}
=I> Minataka kesho twende nikupeleke nyumbani
Nataka kesho twende ukamuone mama x2

BURUDANI:PICHA:CIARA


MICHEZO: MECHI ZA LEO UINGEREZA


HABARI: USWISI "TANZANIA HAINA NIA YA DHATI YA KUCHUNGUZA MABILIONI YALIYOFICHWA NCHINI"

SERIKALI ya Uswisi imesema Serikali Tanzania haijaonyesha nia ya dhati kutaka kuchunguza na kupata mabilioni ya fedha yaliyofichwa na Watanzania katika benki mbalimbali nchini humo.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwananchi Jumamosi, jijini Dar es Salaam jana, Balozi wa Uswisi nchini, Olivier Chave alisema mpaka sasa hakuna jitihada zozote zilizofanywa na Serikali ya Tanzania kutaka ufumbuzi wa tuhuma hizo.
Balozi Chave alisema hayo muda mfupi baada ya kumaliza mazungumzo yake ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe. Hata hivyo wote wawili hawakuwa tayari kueleza ni kipi kilichojiri katika mazungumzo yao.
Katika kikao cha tisa cha Bunge, Novemba mwaka jana, Zitto aliwasilisha hoja binafsi kulitaka Bunge kuchunguza na kuielekeza Serikali kuchukua hatua dhidi ya Watanzania walioficha fedha na mali haramu nje ya nchi.
Katika mazungumzo yake jana, Chave alisema: “Uswisi iko tayari kushirikiana na Tanzania kujua uhalali wa fedha hizo na endapo zikigundulika ni fedha chafu basi tutazirejesha nchini.” Aliongeza:
“Serikali ya Uswisi haina tatizo kwani tumeshafanya hivyo kwa nchi za Ufilipino na Nigeria hivyo tutafurahi na Tanzania kama tutamaliza suala hili”. Alisema habari zinazoandikwa kuhusu mabilioni hayo kuhifadhiwa katika Benki za Uswisi, zinaharibu picha ya nchi hiyo mbele ya mataifa mengine, hivyo angependa suala hilo kumalizwa na kwamba wao wako tayari kusaidia.

Kauli ya Zitto
Kwa upande wake, Zitto alisema hadi sasa Serikali haijamfuata kutaka kutoa ushirikiano wa aina yoyote kuhusu tuhuma hizo.
Alisema kuwa ingawa Serikali ilitaka iachiwe tuhuma hizo ili iweze kuzifanyia kazi, lakini hadi sasa ukimya umetawala.
“Tangu kuahirishwa kwa kikao cha Bunge sijafuatwa na AG (Mwanasheria Mkuu wa Serikali) wala mtu yeyote na sijui kipi kinachoendelea,” alisema Zitto na kuongeza:
“Nitaandika barua na kumkabidhi AG siku ya Jumatatu (keshokutwa ), nitahoji nini kinachoendelea katika uchunguzi huo.”
Zitto ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Naibu Katibu Mkuu Chadema, alisema Serikali ya Tanzania haionyeshi nia ya kuzihitaji fedha hizo. Aliongeza kwamba kuna njia mbili za kuwabaini walioficha mabilioni hayo nchini Uswisi. Kwanza ni kwa Serikali ya Tanzania kushirikiana na Serikali ya Uswisi, pili ni ulipaji wa kodi wa fedha ambazo Watanzania wameweka katika benki nchini humo.
“Njia hii ya pili nayo ni rahisi kwa sababu ukienda kuuliza Uswisi wanaolipia fedha hizo utapata majina yao. Hivyo Serikali itaweza kukamilisha taarifa yake na kuiwasilisha bungeni katika kikao kijacho” alisema Zitto.

Taarifa kutoka Benki Kuu ya Uswisi inaonyesha kuwa baadhi ya fedha hizo zimewekwa katika akaunti za vigogo hao na kampuni za mafuta na gesi zilizopo nchini.

HABARI: MKE AINGIZIWA CHUMA CHA MOTO SEHEMU ZA SIRI NA NA MUMEWE

Mwanamke mkazi wa Kijiji cha Matui, wilayani Kiteto, mkoani Manyara ameponea chupuchupu kuuawa baada ya mume wake kumchoma na chuma cha moto sehemu za siri kutokana na wivu wa mapenzi.
 
Mwanamke huyo alifanyiwa kitendo hicho juzi usiku kwenye kijiji hicho, baada ya mume wake  kumtuhumu kuwa ana uhusiano wa mapenzi na msaidizi wao wa nyumbani.
Akizungumza kwenye Hospitali ya Wilaya ya Kiteto juzi, wakati akipatiwa matibabu mwanamke huyo alisema hivi sasa anasikia maumivu makali.
Alisema alipofanyiwa kitendo hicho alipoteza fahamu kwa muda mrefu, kwani alitokwa na damu nyingi na alizinduka baada ya kufikishwa hospitalini hapo iliyopo umbali wa kilomita 32 kutoka nyumbani kwake.  
Aliongeza kuwa kabla ya kufanyiwa kitendo hicho, kila mara mume wake alikuwa anamweleza kuwa amesikia tetesi kuwa ana uhusiano wa mapenzi na msaidizi wa kazi, hivyo atamfanyia kitu ambacho hatakisahau.
“Siku ya tukio hilo alikoka moto akachukua nondo ya kuweka alama kwenye ng’ombe,  akaniambia ingia ndani mke mwenzako anakuita, nilipoingia ndani naye akaingia na kufunga mlango akaniingiza hiyo nondo ya moto,” alisema.
Daktari wa hospitali hiyo, Godfray Mbise alisema mwanamke huyo amepata kilema cha maisha baada ya kufanyiwa kitendo hicho cha kikatili, kwani ameachiwa majeraha sehemu za siri, mapajani na mgongoni.
Hata hivyo, Diwani wa Kata ya Matui, Kidawa Athuman alisikitishwa na kitendo cha Polisi wa Kituo cha Matui kutochukua jambo hilo kwa uzito.
Athuman alisema askari hao wanashindwa kumchukulia hatua mwanaume aliyefanya kitendo hicho, kutokana na nguvu kubwa ya uchumi aliyonayo.
Pia, alisema kijana huyo msaidizi wa kazi ambaye anahisiwa kuwa alikuwa na uhusiano na mwanamke huyo, naye alichomwa moto sehemu ya taya na alitoroshwa katika maboma ya Kimasai akitibiwe ili kuficha jambo hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Akili Mpwapwa alisema hajapata taarifa za tukio hilo na kwamba, atazifuatilia ikufahamu hatua zilizochukuliwa baada ya kutokea jambo hilo.
“Ndiyo kwanza wewe unanipa habari hizi, ngoja nizifuatilie kisha nitakujulisha kinachoendelea lakini hadi hivi sasa (jana) bado sijapewa taarifa yoyote kuhusiana na kitendo hicho,” alisema Mpwapwa.

MITINDO: MAVAZI YA KIZAZI KIPYA CHA MABINTI





Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...