Language

Friday 8 February 2013

TAARIFA TOKA POLISI MBEYA: HUYU NDIYE ALIYEKUFA AKIGOMBANIA MWANAMKE

MNAMO TAREHE 08.02.2013 MAJIRA YA SAA 06:30HRS HUKO KATIKA MTAA WA ITIJI KATA YA ITIJI JIJI NA MKOA WA MBEYA. DANIEL S/O MWASALEMBA,MIAKA 18,KYUSA,MKULIMA MKAZI WA ITIJI ALIKUTWA AKIWA AMEUAWA  KWA KUCHOMWA KISU KIFUANI UPANDE WA KUSHOTO NA  PETER

MICHEZO: VPL KESHO INAINGIA RAUNDI YA PILI

Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu wa 2012/2013 inaingia raundi ya 16 kesho (Februari 9 mwaka huu) kwa mechi nne ambapo Oljoro JKT itaikaribisha Simba jijini Arusha.

Mechi hiyo namba 129 itafanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid huku Simba ikiingia na kumbukumbu ya sare katika mechi yake iliyopita dhidi ya JKT Ruvu wakati wenyeji wao wakiwa wameshinda 2-0 dhidi ya Kagera Sugar.
Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 3,000 tu utatumika kwa mechi kati ya wenyeji Kagera Sugar na Mgambo Shooting. Mwamuzi wa mechi hiyo atakuwa Amon Paul kutoka Musoma mkoani Mara.
Toto Africans baada ya kufanya vibaya katika mechi

HABARI MUHIMU: MAPENZI YAUA MMOJA KILIMANJARO

WATU wawili wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti mkoani Kilimanjaro likiwemo tukio la mtu kujinyonga kwa kutumia kipande cha kanga.
Katika tukio la kwanza mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Aloyce Msabaha (58), mkazi wa Kibosho Kitandu, Moshi Vijijini alikutwa akiwa amejinyonga kwa kutumia kipande cha kanga na kuacha ujumbe mzito kuhusiana na kifo chake.
Shuhuda wa tukio hilo, aliyefahamika kwa jina la Msabaha ambaye ni baba wa familia ya mke na watoto haifahamiki ilikuwaje mpaka akafikia hatua ya kusitisha uhai wake japo taarifa ambazo hazijathibitishwa zinadai ni wivu wa mapenzi.
Hata hivyo Shuhuda huyo  amesema waulikuta mwili wa marehemu

HABARI MUHIMU: TV 'RUNINGA' HUPUNGUZA NGUVU ZA KIUME!!!

WANAUME wanaotumia muda wa saa tatu na zaidi kwa siku kutazama runinga wanapoteza nguvu za kiume ukilinganisha na wale wanaotazama runinga mara chache.

Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Afya ya Umma cha Havard (HSPH) kilichopo Boston nchini Marekani, umebaini kuwa kuporomoka kwa kiwango cha mbegu za kiume kunahusiana moja kwa moja na kutofanya mazoezi na kutazama runinga kwa muda mrefu.
Imeelezwa kuwa wanaume wanaotazama runinga kwa zaidi ya saa 20 kila wiki wanapoteza asilimia 44 ya mbegu za kiume ukilinganisha na wale wasiotumia muda mrefu katika runinga.

HABARI MUHIMU: BAADA YA ARVs FEKI, HOFU YA DAWA FEKI ZA TB YATANDA TZ

DAWA bandia zinazodaiwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu (TB), zinahofiwa kuingia nchini, ambapo zinadaiwa kutumika kwa kipindi cha zaidi ya miaka miwili tangu mwaka 2011.

Dawa hizo zinazodaiwa kusambaa katika miji mikubwa ya Afrika, zinadaiwa kuanza kuleta madhara kwa watumiaji kwani hazina uwezo wa kuua wadudu wanaosababisha ugonjwa huo.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...