Language

Friday 1 March 2013

BURUDANI: LADY JAY DEE KULETA JOTO NA HASIRA

MWANAMUZIKI wa siku nyingi wa muziki wa kizazi kipya, Judith Wambura Mbibo au Lady Jay Dee, yuko kwenye matayarisho ya albamu yake ya sita, na tayari ameshatengeneza nyimbo mbili, mmoja akiwa amefanya mwenyewe na wa pili akiwa amemshirikisha Profesa Jay, wimbo unaoitwa Joto na Hasira.

  
Jay Dee ambaye pia ni mmiliki wa mgahawa wa Nyumbani Lounge, ameliambia gazeti hili kwamba ujio wake wa safari hii utakuwa wenye ubunifu wa hali ya juu, kutokana na kile anachosema kwamba ana uzoefu zaidi kuliko ilivyo awali na pia anataka kuzikonga nyoyo za wapenzi wake.
Maendeleo ya utengenezwaji wa albamu hiyo yanavyoendelea yatakuwa yakionyeshwa katika kipindi chake cha Diary ya Lady Jay Dee kinachoonyeshwa na kituo cha Televisheni cha EATV.

BURUDANI: PREZZO AMEGOMA KUMUONGELEA GOLDIE


Tangu kurudi kwake Nigeria, na kutengwa kuhudhuria mazishi ya anayedaiwa kuwa mpenzi wake, Goldoe Harvey nyota wa Big Brother toka nchini Kenya, John Makini anayejulikana zaidi kwa jina la Prezzo hajasema lolote kwa vyombo vya habari kuhusiana na majanga yaliyompata huko.


Prezzo, alikuwa Nigeria ambako alikwenda kwa ajili ya Sikukuu ya Wapendanao na kukutana na kifo cha mshiriki mwenzake wa Big Brother na mwanamuziki Mnaijeria, Goldie Harvey ambaye inaaminika walikuwa na uhusiano wa kimapenzi.
Kilichokuja kuibuka na kumchanganya zaidi Prezzo ni mtu anayejulikana kwa jina la Andrew Harvey ambaye aliachia mtandaoni picha za harusi yake na mwanadada Goldie Harvey, ambaye pia siku chache zilizopita alionekana Nigeria akihudhuria mazishi ya mwanadada huyo.
Prezzo kwa upande wake, aliwaambia wanahabari kwamba anahitaji muda wa kupumzika kabla ya kusema lolote.

HILI SWALI NIMEKUTANA NALO FACEBOOK!!!

HABARI MUHIMU: WALIOHUSIKA NA KIFO CHA PADRE UNGUJA WAANZA KUNASWA NA FBI


UJIO wa Askari wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) nchini na kuanza kufanya kazi, umewezesha kuanza kunaswa kwa baadhi ya watu, wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya Padre Evarist Mushi (55) wa Kanisa Katoliki Unguja, visiwani Zanzibar.

HABARI MUHIMU: CHADEMA"HATUWATAKI WAZIRI WA ELIMU NA NAIBU WAKE"

WAKATI Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameunda tume kuchunguza matokeo mabaya ya mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012, Chadema kimesisitiza msimamo wake kwamba kitafanya maandamano kushinikiza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa na Naibu wake, Philipo Mulugo wajiuzulu.

HABARI MUHIMU: KIWANDA CHA GESI MTWARA CHAANZA KUJENGWA


HATIMAYE ujenzi wa kiwanda cha kusafisha gesi kabla ya kusafirishwa kwenda Dar es Salaam umeanza mkoani Mtwara.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi alisema jana kuwa ujenzi huo unaofanywa na Kampuni ya China Petroleum and Technology Development Co-operation (CPTDC), ambao awali, ulipaswa kuanza wiki iliyopita, umeanza juzi baada ya Serikali kufikia mwafaka na wananchi wa Kijiji cha Msimbati kinapojengwa.
“Mkuu wa Wilaya ya Mtwara (Wilman Ndile) na vijana wake walilazimika kufika Kijiji cha Msimbati, ambako wananchi walikuwa na mgogoro na watu wa Marine Park,” alisema Maswi.

HABARI MUHIMU: WANAUME MILIONI 2.8 KUTAHIRIWA MPAKA 2015

SERIKALI imejiwekea lengo la kutahiri wanaume milioni 2.8 ifikapo mwaka 2015, baada ya kufanikiwa kuwatahiri 287,055 kati ya mwaka 2010 na 2012.
Hayo yamebainishwa katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ikifafanua kuwa huduma ya tohara ya kitabibu kwa wanaume ilianzishwa mwaka 2010.
Imetekelezwa zaidi mikoa ambayo ilibainika kuwa na kiwango cha juu cha maambukizi ya virusi vya Ukimwi.
Iligundulika kiwango cha juu cha maambukizi ya VVU ambako kuna kiwango cha chini cha tohara kwa wanaume.  Mikoa hiyo ni ya  Iringa, Njombe, Simiyu, Geita, Katavi, Mbeya, Rukwa,

HABARI MUHIMU: KONDOM FEKI ZINAZIDI KUSAMBAZA MAAMBUKIZI YA HIV/AIDS


WAKATI kondomu feki zilizopigwa marufuku  Uingereza mwaka jana zikiwa katika mzunguko nchini Tanzania, kesi za gonjwa la ngono hatari lisilotibika zimeongezeka kwa asilimia 25 Uingereza, huku wataalamu wakionya kwamba ugonjwa huo umekuwa sugu zaidi katika tiba.
Zaidi ya kesi 21, 000 za maambukizi mapya zimedaiwa kutambulika kwa mwaka 2011/12.
Kondomu hizo feki aina ya Trojan na Durex zenye vipele vipele ambazo mwishoni mwa mwaka jana serikali ya Uingereza iliingia katika msako mkali  kusaka mamilioni ya kondomu hizo bandia zilizokuwa zikiuzwa nchini humo miezi 18 iliyopita.

MICHEZO: KAMA ULIKUWA HUZIJUI, HIZI NDIO MECHI KUBWA ZA LEO DUNIANI MACHI 1


MICHEZO: BENITEZ OUT MEI MWAKA HUU


Rafael Benitez, amesema kuwa atakihama klabu ya Chelsea mwezi Mei mwaka huu na kutaja uamuzi wa kuumpa wadhifa wa kaimu kocha wa klabu hiyo kama kosa kubwa.

Akiongea baada ya kuongoza Chelsea kushinda klabu ya Middlesbrough kwa magoli mawili kwa bila katika mechi ya raundi ya tano ya kuwania kombe la FA, kocha huyo kutoka Uhispania, vile vile aliwashutu mashabiki wa klabu hiyo.
Katika mahojiano na BBC, Benitez amesema uamuzi wa Chelsea wa kuumpa cheo cha

HABARI MUHIMU: OBAMA KUSHIRIKI UAPISHO WA RAIS MPYA WA KENYA


Rais wa Marekani Barack Obama, ni miongoni mwa viongozi wa dunia walioalikwa kwa sherehe za kumuapisha rais wa nne wa Kenya.

Mkuu wa utumishi wa umma, Francis Kimemia amesema kuwa serikali imewaalika Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron na marais wa nchi za Muungano wa Ulaya.

HABARI MUHIMU: HILI NDILO TAMKO LA MWAI KIBAKI KWA UCHAGUZI UJAO


Rais wa Kenya Mwai Kibaki anayehudumu muhula wake wa wisho , amewataka wakenya kuhakikisha kuwa uchaguzi unafanyika kwa njia huru na ya haki watakapokwenda kwenye debe Jumatatu.

MICHEZO: RYAN GIGS ASAINI MKATABA MPYA MANCHESTER UNITED MPAKA 2014

Ryan Giggs mwenye umri wa miaka 39, amesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja na klabu ya Manchester United.


Mchezaji huyo sasa atasalia na Manchester United, hadi juni mwaka wa 2014, na kukamilisha msimu wake wa 23 kama mmoja wa wachezaji kumi na mmoja wa kwanza wa Manchester United.Nahodha huyo wa zamani wa Scotland, alicheza mechi yake ya kwanza na Manchester United tarehe mbili mwezi machi mwaka wa 1991 na maefunga magoli 168 baada ya kucheza mechi

MITINDO: UNAMKUMBUKA FIDELINE IRANGA? HUYU HAPA

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...