Language

Wednesday 6 March 2013

HABARI ZA UCHAGUZI KENYA: MATOKEO KUCHELEWA KUTOKA BAADA YA MITAMBO YA KUHESABIA KUHARIBIKA

Mtandao wa elektroniki wa uwasilishaji na utangazaji wa matokeo ya kura za wagombea urais Kenya umeshindwa kufanya kazi juzi na jana na kuzusha wasiwasi miongoni mwa wananchi.

Mtandao huo ulianza kusuasua tangu juzi mchana na hadi jana mchana ni kura chache tu zilizokuwa zimeongezeka, huku Uhuru Kenyatta wa Jubilee akiendelea kuongoza kwa asilimia 53 dhidi ya Raila Odinga aliyekuwa na asilimia 42 ya kura halali.

HABARI PICHA: HII NILIIKUTA FACEBOOK, NITAIFUATILIA NITHIBITISHE KAMA NI KWELI


HABARI MUHIMU: CHADEMA WAANZISHA TAFRANI KATIKA MAZISHI YA MJUMBE WA CCM


Wafuasi wa Chadema, wameibua tafrani ya aina yake wakati wa mazishi ya aliyekuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), marehemu Benson Mollel baada ya kung’oa bendera za chama hicho na kuamsha hasira za waombolezaji wafuasi wa chama tawala.

Mollel alikutwa amefariki mwanzoni mwa wiki, katika Hoteli ya Lush Garden Business, Mtaa wa Jacaranda Arusha huku mwili wake ukiwa mtupu.Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana na baadhi ya makada wa CCM walionekana wakiwasaka wafuasi hao wa Chadema.

MICHEZO: MATOKEO YA MECHI ZILIZOCHEZWA JANA MACHI 6 KATIKA MASHINDANO MBALI MBALI DUNIANI


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...