Language

Sunday 24 March 2013

HABARI MUHIMU: CHADEMA HAKUNA MAANDAMANO TENA


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimekubali kusitisha maandamano yaliyokuwa yafanyike leo kushinikiza kujiuzulu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne ya 2012.
Makubaliano yalifikiwa baada ya kikao cha Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Said Mwema na viongozi wa Chadema walioongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe kilichofanyika makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...