Language

Tuesday 2 April 2013

LINDSAY LOHAN SI MJAMZITO KAMA ILIVYODHAHANIWA



Lindsay Lohan is not pregnant. Not that we ever really believed she was, but it's good to know for sure, for the sake of the actress and society at large.

The rumor came courtesy of last night's Lindsay Lohan pregnant Tweet, in which the star wrote a simple declaration: "Its official ... pregnant."
Well, it's now official. She was just kidding around.
The 26-year-old star posted on her Twitter April 2:
"April Fools. Where's everyone's sense of humor?"
LL was likely responding to some of the comedic backlash she received, as the Twitterverse largely scoffed at her belated attempt at April Fools humor.
First of all, who posts an April Fools joke at 10:35 p.m. PACIFIC time. Second, pregnancy is not a laughing matter when you're a complete mess at life.
Then again, lateness is a Lohan specialty ... she was an hour tardy to her crucial court hearing, and also missed a flight back to the U.S. from Brazil Monday.
Just be glad her periods have come on time.

KILIMO NA UFUGAJI SIO KAZI YA JINSI MOJA


MSANII WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA SELEMANI MSINDI (AFANDE SELE) ALIPOMWAGA RADHI JUKWAANI


HUYU NDIE MTOTO WA CHEKECHEA ALIYECHINJWA KAMA KUKU MBEYA SIKU YA PASAKA (Samahani kwa picha hii)



MATUKIO ya kutisha na ya kinyama dhidi ya watoto wadogo yameendelea kuutikisa Mkoa wa Mbeya, baada ya mwanafunzi wa chekechea, Ayoub Agen (6) kuuwa kwa kuchinjwa mithili ya kuku na wauaji kuondoka na kichwa chake.

Hata hivyo wananchi wenye hasira walifanikiwa kumnasa mmoja wa watuhumiwa wa tukio hilo, ambaye hata hivyo jina lake halikuweza kupatikana ambapo baada ya kummbana ili aeleze sehemu  walikokificha kichwa cha marehemu aligoma hivyo kuamua kumteketeza kwa moto.
Habari za uhakika kutoka eneo la tukio na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa kijiji cha Ijoka  katika kata ya Mpombo, wilayani Rungwe, Rafael Mwaikenda,  zinadai kuwa tukio hilo lilitokea Machi 31 majira ya saa 11:00 jioni.
Akifafanua zaidi Mwenyekiti  huyo alisema,  marehemu Agen alikuwa ni mwanafunzi wa chekechea katika shule ya msingi Lusanje kijijini hapo na kwamba alikutwa na mauti hayo ya kikatili baada ya watu hao wasiofahamika kufanikiwa kumuiba nyumbani kwao.
Mwaikenda alisema  mwili wa marehemu uliokotwa ukiwa umetenganishwa kichwa na kiwiliwili huku kichwa kikiwa hakionekani hadi sasa ikiwa ni muda mfupi tu baada ya watu hao wasiofahamika kumwiba toka nyumbani kwa wazazi wa marehemu .
Mkazi mwingine katika kijiji hicho, Tumpale Sankemwa, alikielezea mkasa huo, alisema baada ya wananchi kugundua mwili huo wa marehemu waliendelea kuwasaka wahusika na wakiwa katika harakati hizo ghafla walikutana na mtu mmoja ambaye walimtilia mashaka.

MSIMAMO WA LIGI KUU YA UINGEREZA PREMIER LEAGUE


MATOKEO YA MECHI ZA CHAMPIONS LEAGUE NA MECHI NTINGINE KUBWA DUNIANI ZA APRILI 2 YAKO HAPA


KAMA HUKUIPATA HII NDIO HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 MACHI, 2013


Ndugu Wananchi
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uhai na kunipa fursa ya kuzungumza nanyi kwa kupitia utaratibu wetu huu mzuri wa kila mwisho wa mwezi. Leo ninayo mambo matatu ninayopenda kuzungumza nanyi.
Ziara ya Rais wa China Nchini Tanzania
Ndugu wananchi;
Jambo la kwanza ni ziara ya Mheshimiwa Xi Jinping, Rais wa Jamhuri ya Watu wa China aliyoifanya nchini kwetu kati ya tarehe 24 na 25 Machi, 2013. Lengo la ziara yake ilikuwa kuimarisha uhusiano wa kihistoria uliopo kati ya China na Tanzania. Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wakazi wa Dar es Salaam kwa kumpokea vizuri mgeni wetu na ujumbe wake. Wameondoka wakiwa na kumbukumbu nzuri ya nchi yetu na watu wake.

Kwa niaba yenu, nimepokea salamu za shukrani kutoka kwa Rais Xi Jinping akielezea kufurahishwa na mapokezi mazuri tuliyowapatia. Naomba tuendelee kuonesha moyo wa upendo na ukarimu kwa wageni wetu wengine mashuhuri watakaotutembelea siku za usoni.
Ndugu wananchi;
Nami pia, nimemshukuru sana Mheshimiwa Xi Jinping kwa kukubali mwaliko wangu na kufanya ziara ya kihistoria na yenye mafanikio makubwa kwa nchi yetu. Ameifanyia nchi yetu jambo la heshima kubwa na kumbukumbu isiyosahaulika. Tanzania imekuwa nchi ya kwanza Barani Afrika kuitembelea, tena siku kumi tu baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa nchi yake. Na, kubwa zaidi ni kutumia fursa ya ziara yake hapa nchini kutangazia dunia Sera ya China kwa Afrika katika kipindi cha uongozi wake.

BAADA YA BIFU BARIDI NA CLOUDS FM RADIO & TV, SASA LADY JAY DEE KUFUNGUA REDIO YAKE HIVI KARIBUNI


Hatimaye tumepata jibu la kwanini Judith Mbibo aka Lady Jaydee amekuwa akitweet vitu vizito weekend iliyopita. Kama hukufaniwa kuziona tweets hizo ni kwamba mwanadada huyo alishusha mfululizo wa mabomu kuelekea kwa kituo kimoja cha radio na kujikuta akiongeza aka mpya, Anaconda.

Na sasa imebainikiwa kuwa mwanamuziki huyo mkongwe na mjasiriamali anakuja na kituo chake cha radio kiitwacho Kwanza FM. Habari hiyo aliibreak mwenyewe jana na bila shaka haihusiani na April’s Fools Day.

    Kwanza FM coming soon. Yangu mwenyewee

    — Lady JayDee (@JideJaydee) April 1, 2013

Inaonesha kuwa mchakato wa kuanzisha radio hiyo unaenda vizuri kiasi cha kuweka wazi na kuwa hiyo ndio sababu alichukua uamuzi huo wa kuandika mambo ambayo yangeweza kuiharibu career yake ya muziki.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...