Language

Wednesday 3 April 2013

KOREA KUSINI BADO INAENDELEZA MKWARA WA KIVITA



Kufuatia hali hiyo waziri wa ulinzi wa Korea Kusini, ametishia kuwa serikali yake itafanya kila liwezekanalo hata kama ni kutumia jeshi ili kulinda usalama wa raia wa Korea Kusini waliokuwa wakifanya kazi katika eneo hilo ambalo linatumiwa na Korea mbili.

MSIMAMO WA LIGA BBVA


HIKI NDICHO ALICHOKIANDIKA WEMA SEPETU KUHUSU KAJALA MASANJA KATIKA PAGE YAKE YA FACEBOOK


HALI YA NELSON MANDELA SASA INAENDEA VIZURI



Rais mstaafu wa Afrika Kusini Nelson Mandela anaendelea kupata nafuu wakati akitibiwa homa ya mapafu, kwa mujibu wa madaktari wake.

Taarifa kutoka kwa ofisi ya rais Jacob Zuma, ilisema kuwa Mandela alitembelewa na jamaa zake wakati akiendelea kupokea matibabu.
Inaarifiwa kwa sasa hali yake inaendelea kuwa nzuri ikilinganishwa na alivyokuwa wakati alipolazwa hospitalini tarehe 27 mwezi Machi
Mandela amelazwa hospitalini sasa kwa mara ya nne katika kipindi cha miaka miwili.
Mnamo Disemba alitibiwa homa ya mapafu na kibofu na alikaa hospitalini sana kuliko wakatii mwingine wowote.
Mnamo Februari alitibiwa maradhi ya tumbo.
Wiki jana rais huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 94,pia alibitiwa maradhi ya mapafu.
Mpaka sasa hakuna taarifa zozote kuhusu muda atakaosalia kuwa hospitalini.
Bwana Mandela alikuwa rais wa Afrika Kusini tangu mwaka 1994 hadi 1999 na anatazamiwa na wengi kama baba wa taifa hilo kwa kupigana dhidi ya enzi ya utawala wa ubaguzi wa rangi.
Licha ya kufungwa kwa miaka mingi jela, Mandela alisema aliwasamehe maadui zake na kuwataka wananchi wa taifa hilo kushirikiana.
Alishinda tuzo ya amani ya Nobel mwaka 1993

UGANDA IMESITISHA MSAKO WA KIONGOZI WA WAASI WA LRA JOSEPH KONY



Serikali ya Uganda inasema kuwa imesitisha msako wake wa kiongozi mtoro wa waasi wa LRA Joseph Kony, katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati.

Uganda inasema imeamua kuchukua hatua hiyo kufuatia mgogoro wa kisiasa unaokumba taifa hilo baada ya rais Francois Bozize kung'olewa mamlakani.
Pia imeelezea kuwa serikali ya mpito inayoongozwa na kiongozi wa waasi imetatiza shughuli zao.
Uganda inasema kuwa wanajeshi wake katika eneo hilo ambako waasi walichukua mamlaka siku kumi zilizopita, watasalia katika kambi zao hadi muungano wa Afrika utakapotoa mwongozo.
Joseph Kony anayeongoza kundi la waasi wa LRA, anatakikana na mahakama ya kimataifa ya jinai kwa tuhuma za uhalifu wa kivita.
Anaaminika kujificha na wapiganaji wake katika misitu inayopakana na Jamuhuri ya Afrika ya Kati, Sudan Kusini na Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo.

OBAMA NA FAMILIA YAKE MITAANI


HABARI KUBWA ZA APRILI 3 KWA UFUPI



Dozens dead in Afghan court attack Wednesday, April 03, 2013 6:45:00 AM
A suicide bomb and gun attack on a courthouse in the western Afghan city of Farah leave more than 30 people dead and 90 wounded, most of them civilians.
North Korea blocks Kaesong access Wednesday, April 03, 2013 2:27:13 AM
North Korea blocks the entry of South Korean workers into a joint industrial zone, in a move seen as further escalating tensions.
Spain princess gets court summons Wednesday, April 03, 2013 6:58:28 AM
Spain's Princess Cristina gets a court summons - said to be unprecedented - over allegations that her husband misused public money.

SALHA NAE NDANI YA BONGO MOVIE



Mrembo Salha Israel, ambaye alivaa taji la Miss Tanzania mwaka 2011/2012 ameamua rasmi kuingia kwenye tasnia ya uigizaji baada ya msimu wake wa urembo kuisha.

Mrembo huyo amefungua milango yake kuelekea kwenye kazi ya kuigiza filamu za kitanzania kupitia kampuni ya RJ Company katika kazi yake ya kwanza inayoitwa “Bud Luck”, Salha Israel ataonyesha uwezo wake pamoja na wakali wengine kwenye bongomovie kama Batuli na Johari.
Salha ameiambia Mwananchi kwamba amechagua uigizaji kuwa kazi yake mpya kwa sasa, na kwamba mashabiki wategemee mengi kutoka kwake
Akiongeza kwenye mazungumzo hayo Miss Tanzania huyo ambaye alimaliza kutumikia taji lake vizuri bila kupata skendo zozote mbaya alisema,”Kufanya movie ilikuwa ni moja ya ndoto zangu kubwa. Nilikuwa na mawazo kwamba hata ningeshindwa kupata taji la Miss Tanzania basi ningeingia moja kwa moja kwenye uigizaji. Lakini ilinibidi nisubili kidogo baada ya kushinda taji lile na muda ndio huu umefika”.

PINDA AFUNGIA MACHIMBO YALIYOUA ARUSHA



Waziri Mkuu Mizengo Pinda jana alitangaza kuyafunga rasmi machimbo ya moramu eneo la Moshono, Arusha hadi Serikali itakapoweka utaratibu mzuri wa shughuli mbalimbali za uchimbaji katika eneo hilo.

Hatua hiyo ya Pinda imetokana na ajali ya watu 14 waliopoteza maisha baada ya kufukiwa na kifusi juzi, wakati wengine wawili walijeruhiwa kwenye ajali hiyo iliyochangiwa kwa kiasi kikubwa na mvua zinazonyesha jijini Arusha.
Pinda alitoa agizo hilo alipotembelea eneo hilo pamoja na kuwajulia hali majeruhi wawili waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mt Meru.
Majeruhi mmojawapo aliruhusiwa kutoka hospitalini hapo baada ya kuondoka Waziri Mkuu.
Baada ya kuwasili Arusha jana saa 7.30 mchana, Pinda alikwenda moja kwa moja katika Hospitali ya Mt Meru kuwatembelea majeruhi hao.
Wakati wa ziara yake alishuhudia majeneza 14 iliyokuwa na miili ya watu waliofariki kwenye tukio hilo ambayo imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti.
Akizungumza mara baada ya kutembelea eneo hilo Pinda alitoa salamu za pole kwa waathirika kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete huku akilishukuru Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na wananchi waliojitokeza kuokoa maisha ya watu katika tukio hilo. Alisema Serikali imeyafunga machimbo hayo, huku akisisitiza kuwa Serikali kamwe haiwezi kuruhusu uchimbaji wa namna hiyo.

WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AKIPIGA PICHA


JUMA NATURE MWAMBA WA TEMEKE



Mashabiki waliojitokeza kushuhudia mpambano wa Wanaume Halisi na Wanaume Family wamemtunuku Juma Kassim ‘Nature’ kuwa Mfalme wa Temeke kutokana na jinsi walivyomkubali na kumwamini.
Mpambano huo ulioteka hisia za watu wengi, ulipigwa Jumapili iliyopita katika Ukumbi wa Dar Live, Mbagala Zakhem, jijini Dar ambapo mbali na umati mkubwa wa mashabiki hao kumshangilia Juma Nature na kundi lake, walionyesha kukubali onyesho la Wanaume Family walipokuwa jukwaani.
Umati wa mashabiki ulipiga mayowe ya furaha kuonyesha kuwa wamekubali zaidi onyesho la  Wanaume Family kuliko hata lile la Wanaume Halisi haswa walipokuwa wakitumbuiza nyimbo zao zinazopendwaukiwemo Dar Mpaka Moro, Mkono Mmoja,  pamoja na nyingine nyingi kali ambazo walinogesha zaidi walipokuwa wakirusha miguu hewani kwa mtindo wa ‘mapanga shaa’.

SAKATA LA SUMATRA NA NAULI MPYA

Mamlaka ya Udhibiti wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), imepandisha nauli za daladala, mabasi ya kwenda mikoani, usafiri wa reli na tozo za majini kuanzia Aprili 12, mwaka huu.Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Ahmad Kilima alisema jana kuwa nauli za daladala zimeongezeka kwa asilimia 24.46 kwa kuzingatia maoni ya wadau na gharama za uendeshaji.

Kwa upande wa usafiri wa daladala nauli zimepanda kwa umbali tofauti kutoka Sh300 hadi 400, Sh350 hadi 450, Sh500 hadi 600, Sh650 – 750 na kwa wanafunzi kutoka Sh150 hadi 200 katika sehemu yoyote watakayokwenda.
Nauli za usafiri wa mabasi makubwa ya masafa marefu nauli hizo zimeongezeka kwa viwango tofauti. Mathalan kwa basi la kawaida kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya ni Sh30,700, njia ya vumbi kutoka Kigoma hadi Sumbawanga Sh25,400 na basi la hadhi ya kati (Semi Luxury) kati ya Dar na Mwanza ni Sh61,400, wakati basi la hadhi ya juu (Luxury) kati ya Dar na Arusha ni Sh 36,000.
Kilima alisema: “Kuanzia Aprili 12 mwaka huu, kati ya kilometa 0 hadi 10, nauli ya daladala itakuwa Sh400 badala ya Sh300 zinazolipwa hivi sasa.
“Pia nauli za mabasi ya kwenda mikoani zimeongezeka kwa asilimia 20.3 kwa mabasi ya kawaida, mabasi ya kati kwa asilimia 16.9 na mabasi ya daraja la juu kwa asilimia 13.2,” alisema.
Kilima alisema nauli za mabasi ya mikoani zimepanda kutoka Sh30.67 hadi Sh36.89 kwa kilometa kwa mabasi ya daraja la kawaida katika njia za lami.

HIVI NDIVYO MGUU WA STAA WA KIKAPU KEVIN WARE ULIVYOVUNJIKA


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...