Language

Tuesday 16 April 2013

MUHIMBILI KWISHA HABARI YAKE, NI WAGONJWA 7 TU WANAOWEZA KUHUDUMIWA



Kituo cha Afya ya Akili cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kilichopo Chamazi Mbagala kina uwezo wa kuhudumia wagonjwa saba tu imefahamika.

Hali hiyo imekuwa ikisababisha wagojwa wengi wenye tatizo hilo kushindwa kupata huduma au kupata katika hali isiyo na ubora.
Akijibu swali bungeni jana, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Agrey Mwanri, alisema awali kituo hicho kilikuwa na uwezo wa kuhudumia wagonjwa 32.
Mwanari alisema kutokana na kituo hicho kuwa na uwezo wa kuhudumia wagonjwa wachache, Hospitali ya Muhimbili haipeleki wagonjwa katika kituo hicho kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Mwanri alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Mariam Kisangi (CCM), aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kuendeleza kituo hicho ambacho ni muhimu kwa wagonjwa wa akili.

HABARI TOKA BBC, MKENYA MSHINDI WA MBIO ZA BOSTON MARATHON 2012 AELEZEA HOFU YAKE



Mshindi wa mbio za mwaka 2012 za Boston Marathon, Wesley Korir, aliyemaliza wa tano mwaka huu, ameambia BBC kuhusu hofu yake pindi aliposikia milipuko miwili iliyotokea Boston Marekani.
Milipuko hiyo ilitokea karibu na msitari wa mwisho wa kumalizia mbio hizo na kuwajeruhi takriban watu 140 takriban saa mbili baada ya mshindi kumaliza mbio hizo.
''Ikiwa shambulio hilo lingetokea saa mbili kabla ya mbio kumalizika labda ningekuwa miongoni mwa waliojeruhiwa,'' alisema bwana Korir.
Alikuwa akisherehekea ushindi wa mkenya Rita Jeptoo katika mbio za wanawake.
"furaha yetu ni kuwa tulikuwa tayari tumeondoka katika eneo hilo,'' Korir aliambia BBC.
Bi Jeptoo anatoka katika eneo bunge la Cherangany, ambalo bwana Korir ni mbunge wake baada ya kushinda katika uchaguzi uliofanyika mwezi jana.

HII NDIO MECHI YA LEO, ARSENAL VS EVERTON


WATU 16 WAPOTEZA MAISHA MGODINI GHANA



Takriban watu 16 wamefariki baada ya kuangukiwa na mgodi ambao ulikuwa hautumiki nchini Ghana.

Maafisa wanasema kuwa kulikua na maporomoko ya ardhi katika sehemu ambayo ilikua haitumiki karibu na mji wa Kyekyewere ambao una sifa ya kuwa na wachimbaji haramu wa
Waokoaji waliondoa miili 16 baada ya mgodi huo kuporomoka siku ya Jumatatu , kwa mujibu wa maafisa wakuu.
Haijulikani idadi ya watu waliokuwemo ndani ya mgodi huo , lakini inaarifiwa kuwa hukana dalili kuonyesha kuwa bado kuna miili mingine ndani ya mgodi huo.
Ghana ni moja ya nchi kubwa zenye kuzalisha dhahabu hasa baada ya kujulikana kama pwani ya dhahabu.
Afisaa mmoja aliambia shirika la habari la Reuters kuwa mchimbaji mmoja aliyekuwa amejeruhiwa alifariki baadaye hospitalini. Hii inaongeza idadi ya waliofariki hadi 17.
Uchimbaji haramu ni swala linalotela wasiwasi mkubwa nchini Ghana hasa katika maeneo ambako wachimbaji hutumia vifaa vya kisasa kwa shughuli zao.

BARCELONA ANAONGOZA LIGI YA HISPANIA KWA POINTI 81, NA 13 JUU YA REAL MADRID, MSIMAMO WA TIMU ZOTE UKO HAPA


NIMECHELEWA KUYAWEKA MATOKEO YA MECHI KUBWA ZA JANA, LAKINI NAWE UNAWEZA KUWA HUJAPATA MATOKEO YA MECHI ZA JANA, YAKO HAPA


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...