Language

Thursday 18 April 2013

SHIRIKA LA UNICEF NA HOFU YA VIFO VYA WATOTO AFRIKA YA KATI



Shirika la kuwahudumia watoto la umoja wa mataifa UNICEF, limeelezea hofu ya kuongezeka kwa idadi ya watoto wanaouawa katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati.

UNICEF linasema kuwa watoto hao wanajipata katika maeneo ya vita wakati makundi yaliyojihami yanapopambana viwanjani na hata makanisani.
Aidha shirika hilo limesema kuwa takriban watoto watatu waliuawa na wengine zaidi ya ishirini kujeruhiwa vibaya siku ya ijumaa.
Linadai kuwa watoto hao wamesajiliwa kama wapiganaji katika makundi ya waasi.
Kumekuwa na mapigano pamoja na uporaji katika mji mkuu Bangui baada ya waasi kuuteka mji mkuu mwezi jana.

FADHIL MAJIA ARUDI NA KOMBE NCHINI TOKA INDONESIA


HOSNI MUBARAK ARUDISHWA JELA



Aliyekuwa rais wa Misri, Hosni Mubarak, amerejeshwa jela kutoka hospitalini mjini

Shirika la habari la nchini humo MENA limesema kuwa bwana Mubarak alipelekwa hospitalini viungani mwa mji wa Cairo akiwa chini ya uilinzi mkali.
Kiongozi wa mashtaka nchini humo aliamuru Mubarak kurejeshwa jela baada ya kuonekana mwenye nguvu huku akiwapungia mkono wafuasi wake.
Kesi ya mauaji ya waandamanaji dhidi yake itaanzishwa upya mnamo Jumatatu.
Maperma wiki hii mahakama iliamuru Mubarak kutolewa jela baada ya ombi la wakili wake kuwa miaka miwili imepita kabla ya kesi dhidi ya Mubarak kutofanyiwa uamuzi wowote katika kipindi hicho.
Chini ya sheria za Misri mtu hawezi kuwa jela zaidi ya miaka mahakama ikiwa haijatoa uamuzi katika kesi inayomkabili.

RATIBA YA MECHI KUBWA ZA KESHO APRILI 19


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...