Language

Sunday, 31 March 2013

MAHAKAMA "UCHAGUZI KENYA ULIKUWA HURU NA HAKI"


Mahakama ya juu zaidi nchini Kenya, imeamua kuwa rais mteule Uhuru Kenyatta atasalia kuwa rais mpya wa Kenya baada ya kusema kuwa uchaguzi ulifanywa kwa njia huru na ya haki.
Uchaguzi wenyewe ulifanyika tarehe nne mwezi Machi, ambapo hesabu ya kura ilimpa ushindi Kenyatta kwa zaidi ya laki nane.
Rais wa mahakama hiyo jaji mkuu Willy Mutunga alisema kuwa mahakama imekubali kwa kauli moja kuwa uchaguzi ulifanywa kwa njia ya huru na wazi na kuwa Kenyatta na mgombea mwenza wake walichaguliwa kihalali.
Uamuzi huu una maana kuwa Uhuru Kenyatta ndiye ataapishwa kama rais mpya wa Kenya tarehe tisa mwezi ujao
Kesi hiyo iliwasilishwa katika mahakama ya juu zaidi na mpinzani mkuu wa Kenyatta, Raila Odinga baada ya uchaguzi uliofanyika mapema mwezi huu.
Matokeo rasmi yalionyesha kuwa Uhuru alishinda uchaguzi kwa kumpiku Raila kwa asilimia 50.07 huku Raila akipata asilimia 43.28. Matokeo haya yalizuia kufanyika kwa duuru ya pili ya uchaguzi kwa kura 8,100.
Bwana Odinga aliishutumu tume huru ya uchaguzi na mipaka kwa kuhujumu matokeo ya uchaguzi ili kumpa ushindi Uhuru Kenyatta.

US 'PREGNANT MAN' REFUSED A DEVORCE


An Arizona judge has refused to grant a divorce to a transgender man who gave birth to three children.
The judge said there was insufficient evidence that Thomas Beatie was male when he married; the state bans same-sex marriage.
In 2008, Mr Beatie, who had lived as a man for decades, gave birth to a girl, the first of three pregnancies.
He is legally male but kept his female reproductive organs and bore children because his wife was infertile.
A spokesman for Mr Beatie, Ryan Gordon, said Maricopa County Family Court Judge Douglas Gerlach's comments came as a shock. He said his client, who hopes to marry his current girlfriend, planned to appeal the ruling.
"It's unfortunate that the judge out here doesn't recognise marriage in another state,'' Mr Gordon said.

MAITI 22 SASA ZIMEPATIKANA KUTOKA KATIKA KIFUSI DAR ES SALAAM


Idadi ya watu waliokufa kutokana na kufukiwa na kifusi cha jengo la ghorofa 16 lililoporomoka juzi asubuhi jijini Dar es Salaam, imefikia 22.

Habari zilizopatikana kutoka eneo la uokoaji na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova zinaeleza kuwa miili iliyopatikana imepelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Jengo hilo lililokuwa likijengwa mkabala na Msikiti wa Shia Ithnasheri ulioko Barabara ya Indira Gandhi na Kampuni ya Lucky Construction Limited liliporomoka saa 2.30 asubuhi wakati mafundi na vibarua wakiendelea na ujenzi huku chini watoto wakicheza mpira na mama lishe wakiendelea na biashara zao kama kawaida.

Rais Kikwete

Rais Jakaya Kikwete ambaye jana pia alifika katika eneo la tukio, kama ilivyokuwa juzi, alipata taarifa fupi ya maendeleo ya uokoaji kutoka kwa Mkuu wa Mkoa, Said Meck Sadik na Kamanda Kova.

Baada ya kupewa taarifa hiyo, Rais Kikwete alimwagiza Kamanda Kova kuhakikisha wahusika wanakamatwa akiwamo Mkadiriaji Majengo (Quantity surveyor), mchora ramani za majengo (Architecturer), Mhandisi Mshauri (Consultant) na Mhandisi wa Jiji la Dar es Salaam. Juzi baada ya kutembelea eneo la tukio, Rais Kikwete aliagiza wahusika wote wa ujenzi huo wachukuliwe hatua kali.

FIVE DIES IN A HELCOPTER CRASH


Five members of the South African military have died in a helicopter crash, officials said.

The aircraft was patrolling the Kruger National Park on Saturday evening looking for rhino poachers.
The patrol was routine and an investigation is under way.
The poaching of rhinos is rampant in South Africa. Their horns are sold in Asia, where some believe they have medicinal purposes, although there is no evidence to support it.
The South African Broadcasting Corporation quoted Brig Gen Xolani Mabanga as saying that the Agusta A1-0-9 light utility helicopter had come down at around 19:00 GMT on Saturday, killing all five people on board.
Gen Mabanga said the ministry of defence extended condolences to the families of the deceased, all members of the South African National Defence Force.

EASTER MEANS HE LIVES, BONMUSIC BLOG WISH YOU HAPPY EASTER


MSIMAMO WA EPL YA UINGEREZA


MSIMAMO WA LIGA BBVA YA SPAIN


MSIMAMO WA LIGUE 1 YA UFARANSA


MSIMAMO WA LIGI KUU UJERUMANI (BUNDESLIGA)


MATOKEO YA MECHI KUBWA ZA MARCH 30




Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...