
Hata hivyo, chama hicho kikuu cha upinzani kupitia kwa Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Tundu Lissu, kimepinga hatua hiyo kikisema kamati hiyo haipo kisheria kwa mujibu wa Kanuni ya 113(7) kwa kuwa imemaliza muda wake tangu Februari 8, mwaka huu na Spika hajaunda nyingine.