RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Profesa Silas
Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo katika mabadiliko ya
Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.
Kabla ya uteuzi huo, Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda. Ni mmoja wa mawaziri wanaoingiza sura mpya katika Baraza la Rais Kagame ambalo amelifanyia mabadiliko kwa kuunda wizara nyingine mpya.