Language

Wednesday, 13 February 2013

BURUDANI: KUNDI LA MUZIKI LA PAH ONE LAMONG'ONYOKA!!!

Kundi ambalo lilikuwa linaundwa wasanii wanne kwa pamoja likiitwa Pah One sasa limevunjika kwani First Lady wa kundi hilo la Pah One mwanadada Aika ametangaza kujitoa rasmi kwenye kundi hilo pamoja na rapper na producer wa kundi hilo Nahreel na hivyo kundi hilo kubakiwa na wasanii wawili tu. Aika amesema kuwa sababu ya kumfanya ajitoe kwenye kundi hilo ni kutokuwa na maelewano mazuri ndani ya kundi hilo na kuongeza kwa kusema Nahreel ni Solo Artist hivyo yeye na Nahreel hawajavunja kundi hilo na si kwamba mapenzi yake yeye na Nahreel ndiyo sababu iliyopelekea kuvunjika kwa kundi hilo. Nahreel na Aika wanatarajia kuachia ngoma yao ya kwanza wakiwa kama Solo Artists tarehe 14 mwezi huu.

KIBONZO


HABARI MUHIMU: WIFI ANG'ATWA ULIMI MPAKA KUKATIKA

MWALIMU wa Shule ya Msingi Mfaranyaki iliyopo Manispaa ya Songea, Theresia Fuli anashikiliwa na polisi kwa kosa la kumjeruhi kwa kumng’ata ulimi hadi kukatika wifi yake kwa wivu wa mapenzi.

Akizungumza kwa tabu na gazeti hili jana kwenye hospitali ya mkoa alikolazwa wodi daraja la kwanza kwa ajili ya matibabu, majeruhi huyo Oliga Msigale mkazi wa Msamala amesema, bado ana maumivu makali ya ulimi ingawa amepatiwa matibabu.
Amesema siku ya tukio alishangaa kuona anavamiwa na wifi yake ambaye ni mtalaka wa kaka yake, ambapo alimtupia mtoto mkubwa wa kaka yake maharage ya moto kisha kumvamia yeye, huku akimtuhumu kuwa ndiye binti ambaye amechukua nafasi yake bila kujua kuwa yeye ni ndugu wa mume na alipoanguka chini alikabwa koo na alipotoa ulimi nje mwanamke huyo bila huruma alimngata ulimi na kutoa kipande cha ulimi kisha akatoroka eneo hilo.

Tuesday, 12 February 2013

HABARI MUHIMU: POLISI KUWASAKA WOTE WANAOMTUKANA ANNE MAKINDA

POLISI mkoani Dar es Salaam wametangaza kuwafuatilia, kuwasaka na kuwachukulia hatua wote waliotuma ujumbe wa matusi ama kupiga simu ya vitisho kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda.

Viongozi wa Chadema walifanya mkutano wao mwishoni mwa wiki kwenye Viwanja vya Mwembe Yanga, Temeke, jijini Dar es Salaam na kutoa namba za Spika wa Bunge ili mashabiki wamshinikize ajiuzulu.
Pia viongozi hao walitoa namba za simu za Naibu Spika, Job Ndugai ili naye ashinikizwe ang’oke katika nafasi yake kwa madai ya kukandamiza upinzani bungeni.
Chadema walidai kuwa Makinda na Ndugai

HABARI MUHIMU: MKUU WA MAJESHI GUINEA AFARIKI KATIKA AJALI YA NDEGE

Mkuu wa jeshi la Guinea, ameuawa kwenye ajali ya ndege katika nchi jirani ya Liberia, akiwa na maafisa wegine watano.

Generali Souleymane Kelefa Diallom, alikuwa anaongoza wajumbe wa Guinea, katika sherehe za kila mwaka za kuadhimisha siku ya kitaifa ya jeshi la Liberia.
Waliarifiwa kuwa hapakuwa na manusura wa ajali hiyo lakini haikufahamika mara moja idadi ya watu waliokuwa kwenye ndege hiyo.
Baadhi walisema kuwa ni wanajeshi 18 waliokuwa wameabiri ndege hiyo.
Kwa mujibu wa waziri wa habari ,ndege yenyewe ilianguka mjini Charlesville, karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Liberia.
Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirlief, alizuru eneo la ajali, Kusini mwa Monrovia.
Kulingana na shirika la habari la AP, kifo cha Jenerali Diallo, kilitangazwa na rais wa Guinea.
Rais alielezea kusikitishwa na habari za kifo hicho, alipokuwa anakitangaza.

MICHEZO: MECHI ZA LEO KATIKA LIGI YA MABINGWA


Monday, 11 February 2013

HABARI MUHIMU: PAPA BENEDICT XVI AJIUZULU

Huko Ujerumani, msemaji wa serikali amesema kuwa anaheshimu kazi kubwa iliyofanywa na Papa huyu aliyezaliwa katika Jimbo la Bavaria la nchini humo.
 
Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron, amemsifu Papa kwa jitihada zake za kuimarisha mahusiano baina ya Vatican na Uingereza.
Askofu mkuu wa Canterbury amesema amazipokea taarifa za kujiuzulu kwa Papa kwa huzuni mkubwa ingawa anaelewa undani wa hatua yake.
Kiongozi wa Ujeremani, Bi. Angela Merkel amesifu mchango wa Papa wa kupendekeza mjadala baina ya makanisa, waislamu na wayahudi.
Alikumbusha hotuba ya Papa alipozuru bunge la Ujerumani mnamo mwaka 2011.

BURUDANI: HII NDIO SIRI YA NE-YO KUVAA KOFIA MUDA WOTE, 'KIPARA' MUANGALIE KATIKA PICHA HII


MICHEZO: MATOKEO YA MECHI ZOTE KUBWA ZA JANA YAKO HAPA PAMOJA NA RATIBA YA MECHI ZA LEO



MITINDO: NGUO BOMBA KWA BRAZAZ



Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...