WAKATI nchini Zimbabwe wanawake wakitumia pampers kukuza ukubwa
wa makalio yao, nchini Marekani wamekuwa wakitengeneza pampers za
cocaine, ambazo huvaliwa na kusafirisha dawa hizo nchi mbalimbali
pasipo kugundulika.
Mbinu hiyo mpya imedaiwa kuwagharimu muda mrefu
waandaaji kutengeneza pampers hizo na baada ya kukamilika huvaliwa
kitaalamu nje ya nguo zao za ndani na huvalia suruali au baibui tayari
kwa kuanza safari.
Maofisa wa forodha kwenye Uwanja wa Ndege wa JFK
wamegundua mbinu hiyo mpya mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kuwatia
mbaroni wanawake wawili kutoka Bronx wakiwa wamevalia












