Matokeo ya mapema ya uchaguzi wa urais nchini Kenya yanaonyesha Uhuru
Kenyatta ameshinda na kuepuka raundi ya pili ya uchaguzi. Takwimu kutoka tume
ya uchaguzi zinasema Kenyatta ameshinda asilimia hamsini nukta tatu za kura
zote zilizopigwa.
Lakini tume ya uchaguzi itakagua hesabu hiyo kabla ya kutangaza matokeo
baadaye leo jumamosi, siku tano baada yawakenya kupiga kura.








