
Vichwa Vya Habari
Language
Wednesday, 6 February 2013
HABARI MUHIMU: CIA ILISAIDIWA NA NCHI 54 KIUJASUSI
Shirika
la haki za binadamu la Open Society Justice Initiative, limesema mataifa 54
yalisaidia programu za shirika la ujasusi la Marekani CIA, ambapo watuhumiwa wa
ugaidi walifungwa katika magereza ya siri nje ya Marekani, au kukabidhiwa kwa
mataifa ya kigeni kwa ajili ya kuhojiwa.
Shirika hilo limesema
lilichunguza matukio ya ukiukaji wa haki za binaadamu uliohusishwa na magereza
ya siri ya CIA, na operesheni za uhamishaji wa wafungwa baada ya shambulio la
Septemba 11, 2001 mjini New York na Washington. Ripoti ya shirika hilo
iliyopewa jina la "Globalizing Torture" inabainisha kesi za watu 136
na msaada uliyotolewa na mataifa 54. Miongoni mwa mataifa yaliyotuhumiwa
kuisaidia CIA ni pamoja na washirika wa karibu wa Marekani yakiwemo Australia,
Canada, Ujerumani, Uingereza na Ireland, na mengine ambayo yanatizamwa kama
siyo marafiki wa Marekani kama vile Iran.

Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment