Vichwa Vya Habari
Language
Saturday, 19 January 2013
MICHEZO: ARMSTRONG ALILIA KIFUNGO CHAKE CHA KIFO
Mwendeshaji baiskeli Lance Armstrong ameelezea
kushangaa kwa kukabidhiwa adhabu ya maisha ya kutoshiriki katika
michezo, ilhali wanamichezo wenzake wamekuwa wakipigwa marufuku ya miezi
sita tu.
Katika sehemu ya pili ya mazungumzo yake na
Oprah Winfrey, mwanamichezo huyo mwenye umri wa miaka 41 alisema:
"Ninastahili kuadhibiwa. Lakini sidhani ninastahili hukumu ya kifo."
"Ningelitamani sana kupata nafasi ya kushindana, lakini hiyo sio sababu ya yale ninayoyafanya."
Kwa usiku wa pili, mazungumzo yake na Winfrey,
mwenye umri wa miak 58, yalipeperushwa katika muda ambao watazamaji
wengi walipata fursa ya kutizama televisheni, na yalionekana kote
duniani kupitia tovuti yake.Mazungumzo hayo yalikuwa hewani kipitia kituo cha Winfrey cha televisheni nchini Marekani, OWN, yaani Oprah Winfrey Network.
Katika sehemu ya kwanza ya mazungumzo yao, Mmarekani Armstrong hatimaye alikiri kutumia dawa za kuongezea nguvu michezoni zilizopigwa marufuku, baada ya kukanusha kwa muda wa miaka mingi, na huku akiibuka bingwa mara saba wa mashindano ya baiskeli ya Tour de France.
HABARI: WABUNGE 31 WAMEJIANDIKISHA KWENDA JKT
Wabunge vijana katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wameanza kujiandikisha tayari kwa kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa Mujibu wa Sheria kwa ajili ya mafunzo yatakayoanza Machi mwaka huu.
Taarifa zimeeleza kuwa, idadi ya wabunge ambao tayari wamejiandikisha kujiunga na JKT hadi sasa ni zaidi ya 31, huku wengine wakiendelea.
Kujiandikisha kwa wabunge hao ili wajiunge na JKT kunafuatia wito uliotolewa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha, Julai mwaka uliopita, alipowasilisha hotuba ya bajeti ya wizara yake katika Bunge la Bajeti mjini Dodoma.
Kwa nyakati tofauti wabunge vijana kutoka CCM, Chadema na NCCR- Mageuzi walilithibitishia gazeti hili kuwa tayari wamejiandikisha katika Ofisi ya Katibu wa Bunge kwa ajili ya mafunzo hayo.
Imebainishwa kuwa, miongoni mwa wabunge waliojiandikisha, wamo pia ambao waliwahi kupitia mafunzo hayo, ikielezwa kuwa wamefanya hivyo wakitaka kwenda kujikumbushia.
Hata hivyo, Kaimu Katibu wa Bunge, Eliakimu Mrema hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo akieleza kuwa linaweza kuzungumziwa na Spika wa Bunge kwa kuwa ndiye anayezungumzia masuala ya wabunge.
“Sisi kazi yetu ni utendaji tu na masuala ya wabunge, Spika ndiye anayezungumzia,”alisema Mrema.
Alipotakiwa kuzungumzia taarifa hizo, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alisema kwamba ni mapema mno kuzungumzia suala hilo kwa kuwa hawajapata idadi kamili.
“Tukiwa Dodoma (bungeni), ukituuliza tutakuwa tayari kutoa taarifa kamili, lakini kwa sasa ni mapema kuzungumzia suala hilo,”alisema Ndugai na kuongeza:
“Watu ni rahisi kusema, lakini wakati mwingine utekelezaji ni mgumu kama unavyosema kwani, ukisikia moja ya uamuzi mgumu, hili ni mojawapo.”
Ndugai alisema kuwa mafunzo hayo hayatawahusu wabunge ambao waliwahi kupitia JKT siku za nyuma na kwamba ni maalumu kwa wabunge vijana.
“Naomba usubiri Dodoma, tutakuambia hali ilivyo,” alisema Ndugai
Friday, 18 January 2013
MICHEZO: CAPE VEDGE KUFUZU KWA RAUNDI YA PILI ?
Mlinda lango wa Cape Verde, Guy Ramos amesema ana
matumaini makubwa kuwa taifa lake ambalo linashiriki katika fainali hizo
kwa mara ya kwanza litafuzu kwa raundi ya pili kwa fainali.
Ramos amesema ''ikiwa tutacheza mechi hiyo vyema bila shaka watafuzu kwa raundi ijayo''.
Ramos, ambaye anaichezea klabu ya RKC Waalwijk, ya Uholansi, alisema ''kama timu ya nchi ndogo zaidi barani Afrika, hakuna anayetarajia kuwa watashinda mechi yoyote, lakini tulishinda Cameroon 4-0, ambayo ni nchi kubwa na kinyume na matarajio ya wengi tulishinda. Kwa hivyo mbona sisi tusiwashinde Bafana Bafana?''
Thursday, 17 January 2013
HABARI: TIGO IMEGOMA KUPUNGUZA GHARAMA ZA UPIGAJI SIMU
Naibu Mkurugenzi wa Utekelezaji wa Kanda wa TCRA, Victor Nkya, alisema punguzo hilo ni la kutoka asilimia 35 hadi asilimia 69 na kwamba litaanza kutumika Machi mosi mwaka huu
.WAKATI Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikiwasilisha rai ya kupunguza gharama za mwingiliano wa simu , Kampuni ya Tigo imekataa kufanya hivyo kwa madai kuwa itahatarisha uwekezaji wake kwa punguzo la asilimia 69.
.WAKATI Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikiwasilisha rai ya kupunguza gharama za mwingiliano wa simu , Kampuni ya Tigo imekataa kufanya hivyo kwa madai kuwa itahatarisha uwekezaji wake kwa punguzo la asilimia 69.
Msimamo huo wa Tigo, umekuja baada ya TCRA kukutana na wadau wa mawasiliano jana jijini Dar es salaam, ili kukusanya maoni kuhusu mapendekezo ya kupunguza gharama ya mtandao mmoja kwenda mwingine. Hatua hiyo inalenga katika kuwasaidia wananchi kumudu gharama za mawasiliano ya simu.
Naibu Mkurugenzi wa Utekelezaji wa Kanda wa TCRA, Victor Nkya, alisema punguzo hilo ni la kutoka asilimia 35 hadi asilimia 69 na kwamba litaanza kutumika Machi mosi mwaka huu na kukoma Desemba 31 mwaka 2017 .
Nkya alisema punguzo la gharama ya kupiga mtandao mmoja kwenda mwingine kwa mwaka 2013 litakuwa asilimia 34.92, mwaka 2014 asilimia 32.40, mwaka 2015 asilimia 30.18, mwaka 2016 asilimia 28.57 na mwaka 2017 ni asilimia 26.96.
“Lengo letu ni kupunguza gharama za mwingiliano wa simu, mfano mwananchi ambaye yupo Tigo anapiga kwenye mtandao wa Vodacom hizi gharama atazilipa mwenye kampuni ya Vodacom kuilipa kampuni ya Tigo badala ya kulipa mwananchi kama ilivyo sasa,” alisema.
Alisema maoni yanayotolewa na wadau yatachukuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mawasiliano na kuyafanyia kazi.
Alisema maoni yanayotolewa na wadau yatachukuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mawasiliano na kuyafanyia kazi.
Ofisa Mdhibiti wa Kampuni ya Tigo, Levocatus Nkata, alisema punguzo hilo ni kubwa hivyo wawekezaji watashindwa kuendesha kampuni zao.
Alisema Kampuni ya Tigo inatoa huduma zake hadi vijijini na kwamba hatua hiyo itaifanya ishindwe kupeleka na kutoa huduma kwenye maeneo hayo.
Alisema Kampuni ya Tigo inatoa huduma zake hadi vijijini na kwamba hatua hiyo itaifanya ishindwe kupeleka na kutoa huduma kwenye maeneo hayo.
Nkata alisema itachukua muda mrefu kurudisha gharama walizotumia kuendeshea kampuni yao kutokana bei ya kuendesha mitambo.
“Sisi hatukubaliani na hayo mapendekezo yaliyoletwa na TCRA, punguzo hilo kwa sisi wawekezaji ni kubwa sana, tunachoomba wasipunguze ibaki kama ilivyo na kwa mwaka 2017 tunaomba ipunguze kufikia asilimia 45 tu, “alisema Nkata.
Kampuni za Airtel, Vodacom , Benson na Dovetel zimekubali punguzo hilo lakini zimeiomba TCRA ipunguze asilimia chache.
MICHEZO: SUAREZ AKIRI KUJIANGUSHA KATIKA MEHI DHIDI YA STOKE CITY
Msambulizi wa liverpool, Luis Suarez, ana amini kuwa analengwa sana na vyombo vya habari vya Uingereza lakini amekiri alijiangusha katika mechi moja ya ligi kuu msimu huu.
Suarez ambaye ndiye mfungaji bora wa liverpool msimu huu huku akiwa amefunga magoli 15, mawili nyuma ya nyota wa manchester United Robin van Persie, amekiri alijiangusha wakati wa mechi yao na Stoke City tarehe saba October mwaka uliopita.
Tangazo hilo la suarez limemuudhi kocha wa liverpool brendan roggers, ambaye amesema, mchezaji huyo ataadhibiw kuambatana na sheria za klabu hiyo.
Roggers, ametaja tangazo hilo la Suarez, kama moja ambalo kamwe halikubaliki.
MICHEZO: PEP GUARDIOLA AMWAGA WINO BAYERN MUNICH MIAKA 3
Pep Guardiola, mwenye
umri wa miaka 41, awali ilidhaniwa angelijiunga na Chelsea, au Manchester City,
zote za Uingereza.
Guardiola ametia saini
mkataba wa miaka mitatu na Bayern Munich, hadi mwaka 2016.
Atachukua madaraka ya Jupp
Heynckes, ambaye ameamua kustaafu.
Siku zake akiwa mchezaji,
Guardiola, aliwahi kuvichezea vilabu vya Barcelona, Brescia, Roma, Al.-Ahli,
Dorados na pia timu ya taifa ya Uhispania.
Alikabidhiwa pia tuzo nyingi
akiwa mchezaji.
Katika kazi ya meneja,
amewahi kuchukua ubingwa wa ligi kuu ya Uhispania, La Liga, mara tatu, ushindi
wa Supercopa de Espana mara tatu, mara mbili kutwaa ubingwa wa Copa Del Rey,
ubingwa mara mbili wa klabu bingwa barani Ulaya, mara mbili Kombe la Uefa na
vile vile mara mbili ubingwa wa Kombe la Dunia la FIFA kwa upande wa vilabu.
Guardiola, ambaye alizaliwa
tarehe 18 Januari, mwaka 1971, Santpedor, Uhispania, tangu kuondoka uwanja wa
Nou Camp mwezi Mei mwaka 2012, amepumzika msimu mzima, baada ya kukiwezesha
klabu kupata jumla ya vikombe 14, ikiwa ni pamoja na ushindi wa klabu bingwa
barani Ulaya mara mbili.
HABARI: WANAJESHI 200 WA NIGERIA KWENDA KUONGEZA NGUVU MALI
Takriban wanajeshi 200 wa Nigeria wanatarajiwa
kuwasili nchini Mali kusaidia katika harakati dhidi ya wapiganaji wa
kiisilamu Kaskazini mwa nchi.
Jumla ya wanajeshi 3,300 wa kikanda
watapelekwa nchini Mali chini ya azimio la Baraza la Usalama la umoja wa
Mataifa. Chad imesema itapeleka wanajeshi 2,000.
Duru zinasema kuwa makabiliano yalizuka kati ya waasi na wanajeshi mjini Diabaly, umbali wa kilomita 350 kaskazini mwa mji mkuu Bamako siku ya Jumatano.
Subscribe to:
Posts (Atom)








