Language

Thursday 25 April 2013

KURA ZA MAONI KUPIGWA JUU YA AMANI NCHINI MALI


Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kupigia kura azimio linalopendekeza kuundwa kwa kikosi cha kulinda amani nchini Mali.

Kikosi hicho chenye wanajeshi 12,600 kinajumuisha takriban wanajeshi 6,000 kutoka nchi za Magharibi mwa Afrika ambazo tayari zina wanajeshi wao nchini humo.
Azimio hilo limependekezwa na Ufaransa ambayo iliingilia kati mzozo wa Mali mnamo mwezi Januari ili kupambana na wapiganaji wa kiisilamu Kaskazini mwa nchi hiyo.
Kikosi hicho kinatarajiwa kwenda Mali mwanzoni mwa mwezi Julai kabla ya uchaguzi mkuu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...