Language

Friday 5 April 2013

CHADEMA KUMPIGANIA LWAKATARE



Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kwa gharama yoyote kipo tayari kumtetea Mkurugenzi wake wa Ulinzi na Usalama, Wilfred Lwakatare dhidi ya kesi ya ugaidi inayomkabili.

Lwakatare na mwenzake, Joseph Rwezaura, wanakabiliwa na kesi ya ugaidi katika Mahakama ya Kisutu, wakikabiliwa na mashtaka manne ya kula njama na kufanya mipango ya kumteka, kisha kumdhuru kwa sumu, Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mwananchi, Dennis Msacky.
Majalada hayo namba 37 na namba 6 yote ya mwaka 2013, yalishawasilishwa Mahakama Kuu, kwa awamu mbili. Jalada la kwanza, namba 37 liliwasilishwa Mahakama Kuu, Jumatatu na jalada la pili namba 6 liliwasilishwa Jumanne wiki hii iliyopita.
Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa Chadema, Tundu Lissu alisema kuna wanaohoji nguvu ya kisheria wanayoitumia kuweka jopo la mawakili watano kumtetea Lwakatare, akisisitiza kuwa wapo tayari kuhakikisha sheria inatumika ipasavyo kubainisha ukweli wa tuhuma hizo.
Lissu aliyasema hayo jana alipokuwa akieleza msimamo wa baadhi ya mambo yaliyojadiliwa na Kamati Kuu kwenye kikao chake kilichofanyika Dar es Salaam.

MGAMBO MBARONI KWA MAUAJI YA MWENDESHA BAJAJI



Mgambo wa jijini Dar es Salaam (jina linahifadhiwa), anashikiliwa polisi kwa tuhuma za kuhusika katika njama za mauaji ya mwendesha Bajaji Yohana Syprian aliyeuawa jana Kawe jijini Dar es Salaam.

Mgambo huyo ambaye alitambuliwa kuwa ni mlinzi wa maduka ya Bakhresa, inasemekana kutumiwa kama njia ya kumtafuta dereva wa bajaji aliyetuhumiwa kuiba simu hiyo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyera alisema mgambo huyo atahojiwa na kutumika ili kuwapata wahalifu hao.
“Inasemekana marehemu alikuwa ni mpitanjia tu wakati vurugu zinaendelea katika kijiwe hicho, wakaamua kumshambulia yeye mpaka mauti yalipomkuta na baadaye wakamtupa kwenye Mto Mbezi,” alisema Kamanda Kenyera.
Kenyera alisema polisi wanafanya uchunguzi kuhakikisha wanajeshi hao wanaodaiwa kuhusika wanakatwa na kufikishwa mahakamani.
‘‘Huyu mgambo atatusaidia kuwapata kwa urahisi,” alisema na kuongeza: “Si hivyo tu, pia tunawashikilia vijana wengine 12 waliokuwa wanafanya vurugu za kutaka kuchoma moto Kituo cha Polisi.”

UMOJA WA MATAIFA WAIONYA KOREA YA KASKAZINI



Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki moon ameitaka Korea ya kaskazini kupunguza makali yake kwa mzozo unaotokkota wa kinuklia akisema kuwa umeanza kuvuka mpaka.

Bwana Ban amesema kuwa anahuzunishwa na namna ugomvi huo unavyotishia maisha ya wananchi wa kawaida.
Akizungumzia vitisho vya karibuni sana vya Korea Kaskazini kwa Korea Kusini na Marekani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon alisema kuwa hali hiyo imekuwa ya kustajabisha na kusikitisha.
Alisema kuwa Korea Kaskazini imezidisha vitisho vyake na akaonya kuwa cho chote kinaweza kuzusha kitendo cha kusikitisha.
Bwana Ban aliyekuwa wakati mmoja Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Umoja wa Mataifa, alitoa wito kwa viongozi wa Korea kaskazini kubadili mwenendo wao.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...