Language

Sunday 10 February 2013

BURUDANI: DOWNLOAD LET ME LOVE TOU(REMIX) YA NE YO

BURUDANI: LYRICS ZA BOYFRIEND YA JUSTIN BIEBER HIZI HAPA

"Boyfriend"
[Verse 1]
If I was your boyfriend, I’d never let you go
I can take you places you ain't never been before
Baby, take a chance or you’ll never ever know
I got money in my hands that I’d

MICHEZO: NIGERIA MABINGWA WAPYA AFRIKA

Nigeria mabingwa wapya Afrika 2013,yailaza Burkina Faso 1-0 katika mchezo wa fainali nchini Afrika Kusini.

Ni shangwe na vigelegele katika miji mbalimbali nchini Nigeria baada ya timu yao ya The Super Eagles, kuibuka mabingwa wapya wa Kombe la Mataifa ya Afrika.
Mbio za kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika zilizoanza tarehe 19 Januari zimehitimishwa, Jumapili, tarehe 10 Februari kwa Nigeria kuibuka bingwa wa fainali za mwaka 2013 barani Afrika.
Bao la mchezaji Sunday Mba alilofunga katika dakika ya 40 ya kipindi cha kwanza cha mchezo mjini Johannesburg, ndilo lililowahakikishia The Super Eagles, Nigeria kuwa mabingwa wapya.
Mchezo huo ulianza kwa kasi, timu zote mbili zikishambuliana kwa zamu. Hata hivyo Nigeria ndiyo walionekana kutawala zaidi mpambano huo na kukosa magoli kadha ambayo yangeipa ushindi mnono Nigeria.
Wachezaji wa Burkina Faso
Vijana hao wa Super Eagles, wamekuwa wakiimarika kila hatua ya mashindano hayo, hasa baada ya kufuzu kutoka katika makundi. Ni katika hatua ya makundi ambapo mabingwa watetezi, Zambia walitolewa na kuachia kombe hilo kufukuziwa na timu nane zilizoingia robo fainali, na hatimaye timu mbili zilizotinga fainali, Nigeria na Burkina Faso.
Emmanuel Emenike aliibuka mfungaji bora wa mashindano hayo na kupata kikombe, huku Moses Victor akiwa mchezaji bora wa mechi kati ya Nigeria na Burkina Faso.
Mechi hiyo ya fainali ilihudhuriwa na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini, akiwa mgeni rasmi, akiambatana na rais wa Fifa Sepp Blatter na rais wa CAF, Issa Hayatou.
The Super Eagles pia waliahidiwa zawadi kem kem, zikiwemo fedha taslim kwa kocha na wachezaji, hata kabla ya kutwaa ubingwa.
Hii ni zawadi kubwa kwa kocha wa Super Eagles, Stephen Keshi ambaye mwaka 1994, wakati Nigeria ilipotwaa ubingwa wa Afrika, alikuwa nahodha wa timu hiyo katika fainali zilifanyika nchini Tunisia.
Pia Nigeria ilitwaa ubingwa mwaka 1980, wakati fainali hizo zilipoandaliwa nchini Nigeria.
Super Eagles kama ilivyo kwa timu nyingine barani Afrika, itakuwa ikijiandaa kikamilifu kufuzu kucheza fainali za kombe la dunia zitakazofanyika nchini Brazil mwaka 2014.

HABARI MUHIMU: MAJESHI YA MALI YAFIKA GAO

Mapigano baina ya wanajeshi wa serikali ya Mali na wapiganaji wa Kiislamu kwa mara ya kwanza yamefika kati-kati ya mji wa Gao, mji mkubwa kabisa kaskazini mwa nchi.

Mwandishi wa BBC alioko huko anasema wanajeshi wa Ufaransa wanatumia mizinga dhidi ya wapiganaji hao walioingia hapo kabla.
Anasema ghasia zilianza karibu na makao makuu ya polisi, lakini mapigano yametapakaa.
Wanajeshi wa Ufaransa na Mali waliukomboa mji huo mwezi uliopita.
Shirika la habari la Ufaransa linaeleza kuwa wapiganaji wa Kiislamu waliovaa nguo nyeusi, huku wamebeba bunduki, waliteka eneo la kati ya mji wa Gao, mji wenye wakaazi wengi kabisa kaskazini mwa Mali.

MICHEZOl: NIGERIA BINGWA WA AFCON 2013


KIBONZO


HABARI MUHIMU: KAMA HUKUIPATA HII STORI KUHUSU CHANJO MPYA YA UKIMWI, ISOME HAPA

JOPO la Madaktari wa Chuo wa Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), limekamilisha utafiti wa chanjo mpya ya virusi vya Ukimwi, ambao umethibitisha kuwa chanjo ya DNA -MVA ilikuwa salama na yenye uwezo wa kufanya mwili utengeneze kinga dhidi ya virusi vya Ukimwi (VVU).
Utafiti huo ulifanyika nchini kati ya mwaka 2007-2010 na 2008-2012.
Utafiti wa awali uliofanyika kati ya mwaka 2007 hadi 2010, ambao ulijulikana kama HIVIS-03, ulihusisha askari 60 polisi na magereza wa jijini Dar es Salaam, ambao walipewa chanjo hiyo na baadaye kuachwa wakiishi maisha yao ya kawaida kwa muda wa miaka mitano.
Akizungumza na Mwananchi Jumapili, Profesa Muhammad

CHADEMA YAWAKABA KOO MAKINDA NA NDUGAI

VIONGOZI na mashabiki wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana walifanya maandamano na kuhitimishwa kwa mkutano wa hadhara uliofanyika Temeke, jijini Dar es Salaam ambako chama hicho kilitangaza nia ya kuandaa hoja ya kuwang’oa viongozi wa Bunge.
 
Hoja hiyo itawasilishwa katika mkutano ujao wa Bunge kwa ajili ya kuwapigia

MICHEZO: MATOKEO YA MECHI KUBWA ZA LEO UINGEREZA NA HISPANIA BAADA YA HALF TIME



MICHEZO: MSIMAMO WA LIGI KUU UINGEREZA (EPL)


HABARI MUHIMU: UTALII WA NGONO UMEIVAMIA TANZANIA

KATIKA hali ya kawaida, tumezoea kuona watalii kutoka mataifa mbalimbali duniani wakija nchini kuangalia vivutio vya utalii vilivyopo.
Baadhi ya vivutio hivi ni Mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama, majengo ya kale, mapango na nyumba za kihistoria.
Hata hivyo, kumeibuka aina mpya ya utalii, unaojulikana kama utalii wa ngono, ambao unashamiri kwa kasi ukihusisha zaidi watalii wanawake wanaofuata wanaume wa Kitanzania hasa vijana.
Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi Jumapili, unaonyesha kuwa utalii huo unaongezeka kwa kasi hasa katika maeneo yenye vivutio vingi vya utalii ikiwamo Arusha, Kilimanjaro na Zanzibar.

MICHEZO: RATIBA MECHI ZOTE ZILIZOBAKI ZA VODACOM PREMIER LEAGUE IKO HAPA

Februari 13, 2013
Kagera Sugar Vs Coastal Union
Toto Africans Vs Polisi Moro
Mgambo JKT Vs JKT Oljoro
Mtibwa Sugar Vs Ruvu Shooting
African Lyon Vs Yanga SC
Februari 20, 2013
JKT Ruvu Vs Azam FC
TZ Prisons Vs
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...