Language

Wednesday 17 April 2013

BI KIDUDE AFARIKI DUNIA ZANZIBAR LEO MCHANA



Mwimbaji nguli wa muziki wa taarab Fatma Baraka aliyejibebea umaarufu kwa jina la Bi Kidude ameiaga dunia mchana wa leo huko Bububu,  Zanzibar.
Akithibitisha tukio hilo mjukuu  wa marehemu  Fatma Kidude amesema kuwa bibi yake amekutwa na mauti akiwa nyumbani  kwa mtoto wa kaka  yake huko huko Bububu, Zanzibar.
Fatma ambaye pia ni mwimbaji wa kundi la muziki la Gusa Gusa Dar es  Salaam amesema kuwa taratibu za mazishi bado zinaendelea kufanyika wakati mwili wa marehemu  unapelekwa nyumbani kwake Raha  Leo.
Kutokana na taarifa tulizozipata Bi kidude amefariki akiwa na umri wa miaka 103. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi Amen.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...