Language

Wednesday 17 April 2013

HALI YA LADY GAGA INAIMARIKA TARATIBU BAADA YA UPASUAJI WA NYONGA



Mwanamuziki mwenye makeke, Lady Gaga ameendelea kusogeza nyuma ziara ya kutangaza muziki wake ya ‘Born This Way Ball tour’.

Rafiki wa karibu wa msanii huyo amesema kuwa amesogeza nyuma ziara hiyo hadi Septemba mwaka huu,kutokana na hali yake kuwa bado sio nzuri.
“Yupo Chicago chini ya uangalizi wa mpenzi wake Taylor Kinney, ingawa kwa sasa anaendelea vizuri na anaweza kutembea taratibu daktari wake amesema bado anahitaji kupona zaidi”alisema.
Gaga amelazimika kuahirisha ziara hiyo mara mbili kutokana na kuumia nyonga na kufanyiwa upasuaji ambapo hali yake inaendelea vizuri licha ya kuwa bado yupo kwenye uangalizi wa madaktari.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...