Language

Tuesday 29 January 2013

MICHEZO: DROGBA KUICHEZEA GALATASARAY KWA MWAKA MMOJA NA NUSU


Galatasaray imemsajili aliyekuwa mshambulizi wa Chelsea Didier Drogba kutoka kwa klabu ya Shanghai Shenhua inayoshiriki katika ligi kuu ya Premier nchini Uchina.

Galatasaray inayocheza ligi kuu nchini Uturuki, imethibitisha kuwa Drogba amesaini mkataba wa miezi kumi na minane na klabu hiyo.
Mchezaji hiyo mwenye umri wa miaka 34, kwa sasa yuko nchini Afrika Kusini kuiongoza kikosi cha Ivory Coast katika mashindano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika.
Kwa mujibu wa ujumbe uliotumwa na kampuni ya uhusiano bora inayomuakilisha mchezaji huyo Sports PR Company na kuchapishwa kwa mtandano wa kijamii wa Twitter, Drogba alisema anajiandaa kurejea tena katika michuano ya kuwania kombe la klabu binga barani ulaya kwa mara nyingine.
Galatasaray imefuzu kwa raundi ya muondoana ya kuwania kombe hilo na imepangiwa kucheza na FC Schalke 04 kutoka uUjerumani.
''Hii ni fursa nzuri ya kuichezea timu kubwa na ni nafasi ambayo siwezi kupuuza'' Alisema Drogba.

MICHEZO: DONDOO: MARIO BALOTELI KWENDA AC MILAN


BURUDANI: ENRIQUE IGLESIAS-I HAVE ALWAYS LOVED YOU LYRICS

Since the beginning of time
Since it started to rain
Since I heard you laugh
Since I felt your pain
I was too young, you were much younger
We were afraid of each other`s hunger
I have always loved you
There`s never been anyone else
I knew you before I knew myself
Oh my baby,
I have always loved you
Since we kissed the first time
Since we slept on the beach
You were too close for comfort
You were too far

MICHEZO: UPDATES/MATOKEO YOTE YA MECHI ZA JANUARI 29 HAYA HAPA



MITINDO: MAVAZI YANAYO WAFAA WANAWAKE WEMBAMBA




Saturday 26 January 2013

TIBA: DAWA YA KUKUZA NA KUREFUSHA UUME, MAKALIO NA MATITI ISIYO NA MADHARA IMEPATIKANA TZ, HII HAPA

Kwa kutumia mabango, lengo likiwa kutangaza kazi zao, waganga wengi wa tiba asilia wamekuwa wakijinadi kuwa wanatoa tiba ya kurefusha maumbile ya siri ya wanaume, kukuza makalio au matiti.

Katika mitaa ya miji na majiji nchini, siyo jambo la ajabu kukutana na mabango hayo, ambayo hata hivyo kushamiri kwake kunaleta picha kwamba ni kutokana na uhitaji mkubwa wa huduma hiyo nchini, huku watoa huduma husika wakinufaika kwa kujikusanyia kiasi kikubwa cha fedha kutoka kwa wahitaji.
Pia dawa zinazodaiwa kukuza makalio maarufu kama ‘mchina’, zimekuwa gumzo baada ya kuingia nchini, huku zikielezwa kukosa ubora na kwamba zina madhara makubwa.
Lakini, sasa unaweza kuachana na dawa hizo za Kichina, baada ya kugundulika mmea wenye uwezo wa kukuza makalio, matiti, pamoja na kurefusha

BURUDANI:BADO UTATA UMETAWALA!!!

TASNIA ya sanaa ni nyanja ambayo kwa kipindi kirefu imekuwa ikitawaliwa na amani, huku watu wake wakionekana kuwa na furaha na kufanya kazi zao kwa kujitolea zaidi licha ya mapato kiduchu kutokana na kazi zao.

Hata hivyo, kwa takribani

MICHEZO: MECHI ZA LEO KATIKA KOMBE LA MATAIFA GROUP D NA FA CUP ENGLAND



Friday 25 January 2013

HABARI PICHA/BURUDANI: HAPPY 32 YEARS TO MWANADADA ALICIA KEYS


MICHEZO: LIVESCORES UPDATES YA MECHI ZOTE MPAKA SASA IKO HAPA


BURUDANI: LULU KUENDELEA KUSOTA SELO,NI BAADA YA DHAMANA YAKE KUPIGWA KALENDA

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imesogeza mbele tarehe ya usikilizwaji wa maombi ya dhamana ya msanii wa fani ya maigizo, Elizabeth Michael, maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia.

Lulu aliwasilisha mahakamani hapo maombi ya dhamana, kupitia kwa jopo la mawakili wake linaloongozwa na Wakili Kennedy Fungamtama, Makamu wa

HABARI: KESI YA SISTA ALIYEFUMANIWA NA MUME WA MTU SUMBAWANGA KUSIKILIZWA TAREHE 29

KESI  ya  madai  inayomkabili aliyekuwa  Mtawa wa Shirika la Kitawa la Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga, Sista Yasinta Sindani anayedaiwa kufumaniwa na mume wa mtu imepangwa  kusikilizwa Januari 29 mwaka huu.
“Sista’ Yasita  licha ya kuwa mtumishi  wa afya katika  Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini hapa  lakini inadaiwa  ameachana  na maisha  ya  kitawa  miaka  miwili  iliyopita kwa hiyari yake akiwa Mtawa  wa Shirika la  Masista wa Maria Mtakatifu Malkia wa Afrika (MMMA).
Shauri  hilo  la madai  linatarajiwa  kuanza kusikiliza  katika Mahakama ya Mwanzo mjini hapa, mbele ya Hakimu  Jaffari  Mkinga, mlalamikaji Asteria Mgabo anamtaka Yasinta amlipe Sh3 milioni baada ya kumfumania na mumewe wa ndoa aitwaye  Martin Msangawale (39), Mhasibu wa Manispaa ya  Sumbawanga.
Siku hiyo  ya kusikilizwa kwa shauri  hilo  mlalamikaji  katika  shauri  hilo  Asteria  anatarajiwa  kuwaleta  mashahidi wake  wanne mahakamani hapo

HABARI: SITTA KUGOMBEA URAIS 2015

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema kwamba anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania na anafikiria kugombea 2015, iwapo dhamira yake itaridhika na mazingira na upepo wa kisiasa wa wakati huo.
Akizungumza katika mahojiano maalumu, Sitta alitaja mambo kadhaa aliyoeleza kuwa ni ishara ya kukubalika kwake, ikiwamo kuteuliwa na marais wote wanne; Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete katika nyadhifa mbalimbali ikiwamo ya uwaziri.
Kauli ya Sitta imekuja baada ya kuwapo kwa minong’ono ya baadhi ya wananchi kumtaja kuwa miongoni mwa watu wanaoweza kujitokeza kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.
Ni faraja kusikia watu wakinizungumzia kuwa ninazo sifa (za kuwa Rais). Nami ninaamini ninazo sifa. Wakati utakapofika nitajipima. Kama hali hii itaendelea, basi nitaona ni vizuri nigombee,” alisema Sitta ambaye aliwahi kuwa Spika wa

HABARI KUBWA KATIKA MAGAZETI YA LEO: MAKAHABA: HATUTAACHA KUJIUZA NG'O...WAKATI SKENDO CHAFU ZA MASTAA WA FILAMU BONGO ZIMEFIKA KWA JK



BURUDANI: MH. JERRY SLAA MGENI RASMI USIKU WA MASTAA WA FILAMU

Meya wa Ilala Jerry Slaa ndiye atakuwa mgeni rasmi kesho katika Tamasha la Usiku wa Mastaa wa Filamu litakalofanyika katika ukumbi wa kisasa wa burudani Dar Live, Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam. Katika tamasha hilo burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii wa filamu na wale wa Bongo Fleva zitakuwepo

HABARI: JESHI KUCHUKUA UONGOZI UGANDA?

Baada ya sakata la kufariki ghafla mbunge wa chama tawala NRM nchini Uganda,rais Museveni pamoja na waziri wa ulinzi na mkuu wa majeshi wamekuwa wakitoa kauli za kutishia kuliachia jeshi lichukue uongozi nchini humo. 

Nchini Uganda baada ya sakata la wiki kadhaa la kufariki ghafla mbunge wa chama tawala NRM na aliyekuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya chama chake inayoongozwa na Museveni Selina Nambanda,sasa rais pamoja na waziri wa ulinzi na mkuu wa majeshi katika nyakati tofauti wamekuwa wakitoa kauli za kutishia kuliachia jeshi lichukue uongozi nchini Uganda. Yote yanatokana na mpasuko ndani ya chama cha NRM ambapo wabunge wa chama hicho wamekuwa wakitaka ianzishwe tume huru ya kuchuguza kifo hicho,hatua ambayo inapingwa na rais Museveni.Wabunge kadhaa wameshatiwa ndani kufuatia hoja hiyo.Kinachowatia wengi mashaka kwa sasa ni kauli hizo za kutaka jeshi liidhibiti serikali, Saumu Mwasimba amemuuliza mchambuzi wa masuala ya kiasiasa,mhadhiri wa masuala ya sheria katika chuo kikuu cha Makerere,Dkt John Nsokwa anaitazama vipi hatua hii. Kusikiliza mazungumzo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

`MICHEZO: RATIBA YA MECHI ZA LEO KATIKA VIWANJA MBALI MBALI DUNIANI



Thursday 24 January 2013

MAWLID AL-NABI!!!


MICHEZO: KAMA HUKUFANIKIWA KUPATA MATOKEO YA MECHI ZA JANA, HAYA HAPA


MITINDO: KAKAZ MPOOO...HIZI NI PICHA 10 ZINAZOWEZA KUONGOZA MTOKO WAKO WEEKEND HII



BURUDANI: LYRICS ZA PITBULL NA MARC ANTHON-LET IT RAIN OVER ME HIZI HAPA

"Rain Over Me"
(feat. Marc Anthony)

[Marc Anthony]
Girl my body don't lie
I'm outta my mind
Let it rain over me
I'm rising so high
Out of my mind
So let it rain over me

Ay ay ay
Ay ay ay
Let it rain over me

MICHEZO: UPDATES ZA MICHEZO YA LEO ZOTE ZIKO HAPA


MITINDO: FLAVIANA MTATA ASHINDA TUZO YA MWANAMITINDO BORA MWENYE MVUTO ZAIDI AFRIKA

FLAVIANA Matata, mwanamitindo wa kimataifa kutoka Tanzania, ameshinda tuzo ya ‘Nigeria’s Next Super model 2012’ inayomtambulisha kama Mwanamitindo Bora mwenye Mvuto Afrika (Africa’s Most Outstanding Model 2012).

Ushindi wa tuzo hiyo ya pekee kwa aina yake, umefungua milango ya kutambulika zaidi Matata hata kulivusha kimataifa jina la Tanzania katika tasnia ya mitindo na mavazi.
Akiongelea ushindi wa tuzo hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Compass Communication Tanzania Limited, Maria Sarungi Tsehai alisema ushindi wa Matata ni mafanikio mengine ya kujivunia. Tsehai ndiye aliyevumbua kipaji cha Matata.
Kwa mara ya kwanza Flaviana aliibuka kwenye mashindano ya Miss Universe akiweka rekodi ya mrembo wa kwanza kushinda taji hilo nchini.
Aliiwakilisha nchi kwenye mashindano ya ‘World Miss Universe’ mwaka 2007 na kumaliza nafasi ya sita, mjini Mexico City, Mexico.
Matata pia ni balozi wa taasisi ya kusaidia watoto (SOS) na Matata Diamond Empowerment Fund (Def) ya Marekani, ambapo anafanya kazi sambamba na mwanamitindo na msanii wa vipindi vya televisheni Kim Kardashian.
Kimwana huyo pia ana mkataba na kampuni ya mitindo ya Afrika Kusini inayojulikana kama Boss Models SA, ambapo awali pia aliwahi kufanya kazi na

BURUBANI: CHRIS BROWN-DON'T JUDGE ME LYRICS (IMEOMBWA NA HAJI RAMADHANI VIA FACEBOOK)

Verse 1:
I don't wanna go there
We should never go there
Damn why you wanna go there
I guess I gotta go there
You're hearing rumors about me
And you can't stomach the thought
Of someone touchin my body

BURUDANI: HOW DEEP IS YOUR LOVE LYRICS, SEAN PAUL FT. KERRY RAWLAND



[Sean Paul:]
Bada bang bang bang
Late by the King call
Over is all our brain
Baby girl, Listen what me sing yeah
Badabang, Bada bang bang bang ban
Sean Da Paul him ah the Don
Yo, girl just hold my hand,
I gotta let you know I am the man

Girl cause the way how ah wine,
And ah bubble it, bubble it

BURUDANI: ANGALIA PICHA 4 ZA MKE WA MTU AKIFANYA UCHAFU UKUMBINI

KITUKO cha aina yake kimejiri Jumamosi iliyopita ndani ya Ukumbi wa Meeda Sinza jijini Dar wakati Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo’ ilipokuwa ikitumbuiza.





HABARI PICHA: HII NYUMBA NI.....HEBU ICHEK MWENYEWE


MITINDO: LEO TUFOCUS VIATU VIREFU VYA KIKE


MICHEZO: RATIBA YA MECHI ZA LEO KATIKA VIWANJA MBALI MBALI DUNIANI


HILI NDILO TAMKO LA KANISA LA MORAVIAN KUSINI

Halmashauri Kuu ya Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini na bodi ya wadhamini wa mali za kanisa hilo, wametoa tamko zito la kumtaka Mwenyekiti wa Jimbo la Misheni Mashariki aliyesimamishwa, Mchungaji  Clement Fumbo kurudisha mali za kanisa na kuacha kujihusisha na shughuli za kanisa hilo.

Tamko hilo limekuja kufuatia Mchungaji Fumbo kujihalalisha siku za hivi karibuni kwamba yeye ni Mwenyekiti halali wa Jimbo la Misheni, ikiwa ni pamoja na kutangaza viongozi wapya wa halmashauri kuu jambo lililolenga kuwagawa waumini ndani ya kanisa hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Jimbo la Kusini, Clement Mwaitebele alisema alichokifanya Mchungaji  Fumbo ni ubatili mkubwa na kwamba ni kitendo kinachohatarisha amani ya Watanzania, hivyo kama viongozi wakuu wa kanisa wameamua kuingilia kati.
Alisema barua za kumtaka afanye hivyo tayari zimeshaandaliwa na kwamba akikaidi kurudisha ofisi, kuondoka katika Jengo la Usharika wa Tabata na

Wednesday 23 January 2013

HABARI: HAYA NDIO MATOKEO YA UCHAGUZI ISRAEL

Wapiga kura wa Israel wamemuondowa patupu waziri mkuu Netanyahu anaekabiliwa na kazi ngumu kuweza kuunda serikali ya muungano 

Waisraeli wamepiga kura jana, na wamezusha maajabu. Mtangazaji wa zamani wa televisheni, Jair Lapid na chama chake cha kiliberali - Yesh Atid - amemaliza nafasi ya pili akijikingia viti 19 vya bunge la Knesset. Yeye ndiye mshindi mkubwa wa uchaguzi huo. Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ameondolewa patupu na wapiga kura. Muungano wa vyama vya mrengo wa kulia vya Likud na Beitenu, anaouongoza, umejipatia viti 31 toka jumla ya viti 120 vya bunge la Israel - Knesset.
Baada ya ushindi kama huo, kimsingi mshindi hupanda ndani ya gari la fakhari

HABARI:WATU 23 WAMEUAWA NIGERIA KATIKA MASHAMBULIZI TOFAUTI

Washukiwa wa kundi la wapiganaji wa kiisilamu , wamelaumiwa kwa mauaji ya watu 23 katika mashambulizi tofauti Kaskazini mwa Nigeria
.
Walio shuhudia mauaji hayo wanasema kuwa washambuliaji waliwalenga watu waliokuwa wanauza nyama ya wanyamapori, katika eneo la Damboa siku ya Jumatatu na kuwaua watu 18.
Watu wengine watano walifariki Jumanne wakati kundi la wanaume waliokuwa wanacheza mchezo wa kamari walishambuliwa mjini Kano.
Kundi la Boko Haram, linalopigana kutaka kuweka sheria za kiisilamu, nchini Nigeria limekuwa likifanya mashambulizi, katika sehemu kadhaa nchini humo.
Boko Haram imelaumiwa kwa vifo vya takriban watu 1,400,

HABARI: SASA NI ZAMU YA CHADEMA KUIRARUA CCM

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimejibu CCM kuhusu kauli zake za hivi karibuni kuwa Chadema itakufa.Akihutubia Mwanza hivi karibuni, Nape Nnauye alikaririwa akisema Chadema itakufa kutokana na laana ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na kwamba ni chama kilichojaa ubaguzi.
Akijibu kauli hiyo jana, Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema, Benson Kigaila alisema chama hicho hakiwezi kulumbana na Nape.
Kigaila alisema Chadema haina makundi na haitakufa kwa laana ya Mwalimu Nyerere.
Tunataka kuwaambia kuwa Chadema haina ubaguzi hivyo haiwezi kufa leo wala kesho mpaka iwe imetimiza kazi yake ya kuwakomboa Watanzania. Kama ni suala la Mwalimu Nyerere, laana hiyo iko ndani ya CCM yenyewe,” alisema.
Akitaja sababu za kudai kuwa laana imo ndani ya CCM, Kigaila alisema chama hicho kimevunja umoja wa kitaifa uliojengwa na Mwalimu Nyerere na kwamba, alitunga kitabu kuwa CCM imeoza na kinanuka rushwa.
Aliongeza kuwa CCM ina laana ya Mwalimu kwa sababu imerasimisha ubaguzi kwa viongozi wanachama wao.
Ni haohao CCM wanaosema Chadema kina ukabila waliomzushia Dk Salim Ahmed Salim uongo kuwa ni Mwarabu na alihusika na kifo cha aliyekuwa mmoja wa waasisi wa taifa hili, Abeid Karume. Uchafu uliofanywa na wanamtandao,” alisema Kigaila.
Aliendelea kuituhumu CCM kwa kukandamiza haki za wafanyakazi, huku akitoa mfano wa tukio la kutekwa na kuteswa kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania (Mat), Dk Steven Ulimboka.
Pia, alitoa mfano wa wazee waliostaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao wanaodai mafao yao hadi leo, wakati Serikali ya Uingereza ilishalipa fedha zao tangu jumuiya ilipokufa mwaka 1977.
Kuhusu hatua ya kuwavua uanachama, baadhi ya viongozi wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), Kigaila alisema chama hicho hakitavumilia makosa kama uzembe, ufisadi, udhaifu, ubadhirifu na usaliti.

Amshukia Mwigulu Nchemba
Pia, Kigaila alimshambulia Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Mwigulu Nchemba kwa madai kuwa, tuhuma alizotoa dhidi ya Chadema kwamba kinapanga mauaji, zinaidhalilisha Serikali na polisi.
Alimtaka Nchemba kupeleka ushahidi wa tuhuma zake kwenye vyombo vya sheria badala ya vyombo vya habari. “Tunataka kumwambia Rais Jakaya Kikwete, Mkuu wa Polisi, Said Mwema na Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Othman Rashid kuwa ukimya wao... ni tafsiri kuwa polisi sasa inafanya kazi kwa kufuata amri za Chadema,” alisema Kigaila.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...