Language

Friday 26 April 2013

KOCHA WA YANGA KWENDA AMAVUMBI YA RWANDA?


KOCHA Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts ni kati ya makocha wanaopewa nafasi ya kuwania nafasi ya kuifundisha timu ya taifa ya Rwanda ‘Amavubi’.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Shirikisho la Soka la Rwanda (Ferwafa) zimeeleza, Brandts ni kati ya wanaopewa nafasi ikiwa ni siku chache baada ya aliyekuwa Kocha Mkuu Sredojevich Milutin ‘Micho’ kufukuzwa kazi.
Micho raia wa Serbia aliyewahi kuwa kocha wa Yanga alitupiwa virago baada ya timu hiyo kufanya vibaya kwa miezi minne mfululizo.
Brandts raia wa Uholanzi, amekuwa akipewa nafasi hiyo baada ya kamati ya ufundi ya Ferwafa kutoa pendekezo kutokana na mafanikio aliyoyapata wakati akiwa nchini Rwanda akiinoa APR.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...