Language

Friday 26 April 2013

BARACK OBAMA ATOA ONYO KWA SYRIA


Rais wa Marekani Barrack Obama, ametoa onyo jipya kwa Syria kwamba matumizi ya silaha za maangamizi makubwa dhidi ya raia nchini humo huenda likapelekea kubadilisha msimamo wa Marekani juu ya kuingilia kijeshi Syria. 

Obama ametoa onyo hilo wakati akiwa anakabiliwa na shinikizo kutoka nchini mwake na bara la ulaya kwa ujumla kuingilia mapigano ya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria.
Hata hivyo siku moja baada ya Marekani kusema kwamba kemikali hizo zenye sumu huenda zimetumika kwa kiwango kidogo, Obama anasema nchi yake lazima iwe na uhakika wa matumizi ya silaha za kemikali, na ushahidi unaoonyesha silaha hizo zimetumika kivipi na wapi.
" Tumeshawahi kuona picha mbaya sana zamani, baada ya maafisa wa ulinzi wanaoonekana kufanya maamuzi kutokana na maswala ya sera, na baadaye inakuja kubainika kuwa ushahidi iliopelekea maamuzi hayo kufanywa si wa ukweli ," alisema afisa mmoja wa ulinzi nchini Marekani ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Afisaa huyo alikuwa akitoa mfano wa namna Marekani ilivyoiingilia kijeshi nchini Iraq baada ya kugundua kuwa silaha za maangamizi yenye nguvu zinatumika katika ghasia za nchi hiyo madai ambayo baadaye yalisemekana sio ya kweli. Katika ghasia hizo za mwaka 2003, wanajeshi 4,500 wa Marekani waliuwawa huku raia wengi wa Iraq pia wakipoteza maisha yao.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...