Vichwa Vya Habari
Language
Tuesday, 26 March 2013
MITINDO: FLAVIANA MATATA ATUMIKA KATIKA UTAPELI
KAMPUNI ya Compass Communications imewatahadharisha warembo na
wanamitindo wote nchini kutorubuniwa na genge la watu wanaotumia jina la
Flaviana Matata kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Labels:
HABARI MUHIMU,
MITINDO
BURUDANI: P SQUARE"HATUWEZI BILA MAMA"
Wakali wa ngoma za Alingo na Beautiful Onyinye, Peter na Paul Okye
wanaounda kundi la P-Square, wametoa sababu inayowafanya wachukue muda
mrefu kutoa albamu mpya kuwa ni kukosekana kwa sapoti ya mama yao ambaye
alifariki dunia Julai 13 mwaka jana.
Mapacha hao wamesema kuwa kabla mama yao hajafariki Dunia alikuwa
pamoja nao studio walipokuwa watengeneza albamu na alikuwa akiwaombea wiki
nzima kabla ya kuingiza albamu sokoni na hawajui kwa sasa itakuwaje.
“Alipokuwa hai alikuwa ni sehemu ya mafanikio yetu hasa kipindi ambacho
tunaandaa albamu alikuwa akikesha nasi studio na kuombea hata kazi zetu lakini
sasa maisha yamekuwa magumu na sijui tutafanyaje albamu tutakapokuwa tayari
kuifanya”walilalamika wasanii hao.
Akifafanua zaidi Peter alisema kuwa mama yao alikuwa ni muumini mzuri
na alikuwa na kanisa lake ambalo walishirikiana kulijenga tunachofanya kumuenzi
ni kuhakikisha linaendelea.
Labels:
BURUDANI
HABARI MUHIMU: MASHEIKH WA UAMSHO SASA WAKABILIWA NA MASHTAKA MAPYA
Washtakiwa wa kesi inayowakabili viongozi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara
ya Kidini (Jumiki) Zanzibar, wamesomewa mashtaka mapya katika Mahakama Kuu.
Labels:
HABARI MUHIMU
HABARI MUHIMU: SASA NA CHADEMA VS OCD ARUSHA
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini,
kimetangaza mgogoro na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo na Kamanda wa
Polisi Wilaya ya Arusha (OCD), Gilles Bilabaye .
Hatua hiyo inatokana na kile kinachodai walitumia lugha na kauli za matusi dhidi ya wanachama na wafuasi wa chama hicho, kwenye harakati za kuzuia maandamano yaliyoitishwa kumshinikiza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa ajiuzulu.
Akisoma tamko la chama hicho kwa waandishi wa habari jana, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema viongozi hao waliwaita vijana wafuasi wa Chadema kuwa ni wahuni, wavuta bangi na wanywa viroba.
Pia, wanadaiwa kuwaita wafuasi hao kuwa hawana kazi za maana, ndiyo maana wanakubali kushiriki maandamano yanayoitishwa na chama hicho.
“Tunatoa muda wa siku tatu kwa viongozi hao kutumia njia ileile ya redio za masafa mafupi Arusha na magari ya matangazo walizotumia kutoa matusi hayo, kuomba radhi kwa vijana wa Arusha,” ilisema taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu wa Kanda hiyo, Amani Golugwa.
Labels:
HABARI MUHIMU
HABRI MUHIMU:CHETI CHA MULUGO BADO UTATA
Imebainika kuwa mmoja wa watu ambao Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya
Ufundi, Philipo Mulugo (pichani)anadaiwa kutumia jina lake kutafuta kazi ya
ualimu katika Shule ya Sekondari ya Southern mkoani Mbeya ni Mhadhiri katika
Chuo Kikuu kishiriki cha elimu Mkwawa (Muce), kilichopo mkoani Iringa.Mhadhiri huyo ni Dick Aron Mulungu ambaye alisoma na Mulugo katika Shule ya Sekondari ya Songea Wavulana kati ya 1994 na 1996 na alijiunga na shule hiyo baada ya kuhitimu kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Kafule, ambayo iko mkoani Mbeya.
Labels:
HABARI MUHIMU
Monday, 25 March 2013
HABARI KWA UFUPI: STORI 10 KUBWA ZA LEO DUNIANI
Cyprus bailout remarks alarm markets Monday, March 25, 2013
11:43:03 AM
European and US stock markets reverse early gains and head lower, despite the agreement of a bailout deal for Cyprus.
European and US stock markets reverse early gains and head lower, despite the agreement of a bailout deal for Cyprus.
US army hands over Bagram prison Monday, March 25, 2013
10:01:07 AM
The US army hands over to Afghanistan the notorious Bagram jail, resolving an issue that has strained ties between the countries.
The US army hands over to Afghanistan the notorious Bagram jail, resolving an issue that has strained ties between the countries.
EU suspends most Zimbabwe sanctions Monday, March 25, 2013
8:59:39 AM
The European Union suspends sanctions against 81 officials and eight firms in Zimbabwe following what it called a "successful" constitutional referendum.
The European Union suspends sanctions against 81 officials and eight firms in Zimbabwe following what it called a "successful" constitutional referendum.
Labels:
HABARI KWA UFUPI
Sunday, 24 March 2013
HABARI MUHIMU: CHADEMA HAKUNA MAANDAMANO TENA
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimekubali kusitisha
maandamano yaliyokuwa yafanyike leo kushinikiza kujiuzulu Waziri wa Elimu na
Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha
nne ya 2012.
Makubaliano yalifikiwa baada ya kikao cha Mkuu wa Jeshi la Polisi
Tanzania (IGP), Said Mwema na viongozi wa Chadema walioongozwa na Mwenyekiti wa
Chama hicho, Freeman Mbowe kilichofanyika makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar
es Salaam.
Labels:
HABARI MUHIMU
Subscribe to:
Posts (Atom)





