Language

Tuesday, 26 March 2013

NYOTA WA FILAMU TZ, IRENE UWOYA


ISIKILIZE NA UICHUKUE HAPA MIRRORS YA JUSTIN TIMBERLAKE MP3

MITINDO: FLAVIANA MATATA ATUMIKA KATIKA UTAPELI


KAMPUNI ya Compass Communications imewatahadharisha warembo  na wanamitindo wote nchini kutorubuniwa na genge la watu wanaotumia jina la Flaviana Matata kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

BURUDANI: P SQUARE"HATUWEZI BILA MAMA"


Wakali wa ngoma za Alingo na Beautiful Onyinye, Peter na Paul Okye wanaounda kundi la  P-Square, wametoa sababu inayowafanya wachukue muda mrefu kutoa albamu mpya kuwa ni kukosekana kwa sapoti ya mama yao ambaye alifariki dunia Julai 13 mwaka jana.


Mapacha hao wamesema kuwa kabla mama yao hajafariki Dunia alikuwa pamoja nao studio walipokuwa watengeneza albamu na alikuwa akiwaombea wiki nzima kabla ya kuingiza albamu sokoni na hawajui kwa sasa itakuwaje.
“Alipokuwa hai alikuwa ni sehemu ya mafanikio yetu hasa kipindi ambacho tunaandaa albamu alikuwa akikesha nasi studio na kuombea hata kazi zetu lakini sasa maisha yamekuwa magumu na sijui tutafanyaje albamu tutakapokuwa tayari kuifanya”walilalamika wasanii hao.
Akifafanua zaidi Peter alisema kuwa mama yao alikuwa ni muumini mzuri na alikuwa na kanisa lake ambalo walishirikiana kulijenga tunachofanya kumuenzi ni kuhakikisha linaendelea.

HABARI MUHIMU: MASHEIKH WA UAMSHO SASA WAKABILIWA NA MASHTAKA MAPYA


Washtakiwa wa kesi inayowakabili viongozi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kidini (Jumiki) Zanzibar, wamesomewa mashtaka mapya katika Mahakama Kuu.

HABARI MUHIMU: SASA NA CHADEMA VS OCD ARUSHA


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini, kimetangaza mgogoro na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo na Kamanda wa Polisi Wilaya ya Arusha (OCD), Gilles Bilabaye .


Hatua hiyo inatokana na kile kinachodai walitumia lugha na kauli za matusi dhidi ya wanachama na wafuasi wa chama hicho, kwenye harakati za kuzuia maandamano yaliyoitishwa kumshinikiza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa ajiuzulu.
Akisoma tamko la chama hicho kwa waandishi wa habari jana, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema viongozi hao waliwaita vijana wafuasi wa Chadema kuwa ni wahuni, wavuta bangi na wanywa viroba.
Pia, wanadaiwa kuwaita wafuasi hao kuwa hawana kazi za maana, ndiyo maana wanakubali kushiriki maandamano yanayoitishwa na chama hicho.
“Tunatoa muda wa siku tatu kwa viongozi hao kutumia njia ileile ya redio za masafa mafupi Arusha na magari ya matangazo walizotumia kutoa matusi hayo, kuomba radhi kwa vijana wa Arusha,” ilisema taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu wa Kanda hiyo, Amani Golugwa.

HABRI MUHIMU:CHETI CHA MULUGO BADO UTATA


Imebainika kuwa mmoja wa watu ambao Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo (pichani)anadaiwa kutumia jina lake kutafuta kazi ya ualimu katika Shule ya Sekondari ya Southern mkoani Mbeya ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu kishiriki cha elimu Mkwawa (Muce), kilichopo mkoani Iringa.

Mhadhiri huyo ni Dick Aron Mulungu ambaye alisoma na Mulugo katika Shule ya Sekondari ya Songea Wavulana kati ya 1994 na 1996 na alijiunga na shule hiyo baada ya kuhitimu kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Kafule, ambayo iko mkoani Mbeya.

Monday, 25 March 2013

HABARI KWA UFUPI: STORI 10 KUBWA ZA LEO DUNIANI


Cyprus bailout remarks alarm markets Monday, March 25, 2013 11:43:03 AM
European and US stock markets reverse early gains and head lower, despite the agreement of a bailout deal for Cyprus.
US army hands over Bagram prison Monday, March 25, 2013 10:01:07 AM
The US army hands over to Afghanistan the notorious Bagram jail, resolving an issue that has strained ties between the countries.
EU suspends most Zimbabwe sanctions Monday, March 25, 2013 8:59:39 AM
The European Union suspends sanctions against 81 officials and eight firms in Zimbabwe following what it called a "successful" constitutional referendum.

BURUDANI: LISTEN/DOWNLOAD GOOD KUSH & ALCOHOL {Bitches Love Me} Feat. DRAKE [Prod. By Mike Will Made It]

Sunday, 24 March 2013

HABARI MUHIMU: CHADEMA HAKUNA MAANDAMANO TENA


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimekubali kusitisha maandamano yaliyokuwa yafanyike leo kushinikiza kujiuzulu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne ya 2012.
Makubaliano yalifikiwa baada ya kikao cha Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Said Mwema na viongozi wa Chadema walioongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe kilichofanyika makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...