Language

Monday 21 January 2013

HABARI: MATEKA 37 TOKA NCHI 8 WALIUAWA ALGERIA

Waziri mkuu wa Algeria Abdelek Sellal amesema mateka 37 wa kigeni kutoka nchi 8 za kigeni waliuawa katika makabiliano ya watekaji nyara na jeshi.
Katika taarifa yake wazieri mkuu alisema kuwa raia mmoja wa Canada ni miongoni mwa wapiganaji walioteka kiwanda cha gesi na kuwakamata mateka.
Alisema kuwa watekaji nyara 29 waliuawa na wengine watatu walikamatwa wakiwa hai.
Tukio hilo lilifika kikomo siku ya Jumapili . Inaaminika mateka zaidi ya 45 wakiemo raia wa Algeria waliuawa.
Wanajeshi wanaendelea na upekuzi katika eneo kulipotokea utekaji nyara katika kiwanda cha mafuta cha Amenas. Ndani ya kiwanda hicho zaidi ya maiti ishirini zilizoteketea kiasi cha kutoweza kutambulika zilipatikana.
Taarifa zaidi zinaarifu kuwa Maiti za mateka kutoka Japan, Norway, Uingereza, Marekani na Malaysia bado hazijatambuliwa huku maafisa wa usalama wakisema kuwa watekaji nyara watano tayari walithibitishwa kuuawa na wapiganaji.


No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...