Language

Friday 11 January 2013

MICHEZO: NIGERIA KUSHINDA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA 2013?

Wacheza kamali wanataka kucheza karata zao vizuri kuhusu kinyang'anyiro cha ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2013.

 
Wacheza kamali hao wataelekeza karata yao katika timu ya Nigeria wakiipa nafasi ya kuwa katika timu tatu bora za juu.

Timu ya Nigeria, The Super Eagles, imeshiriki mara 16 katika mashindano ya kombe hilo na kushinda mara mbili, ikishika nafasi ya pili mara nne na mara saba katika nafasi ya tatu, ikiwa ni rekodi ya kujivunia katika kipindi cha miaka 50.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...