Language

Monday 18 March 2013

AFYA: TUMIA VEMA VYOMBO VYA MAWASILIANO KULINDA AFYA YAKO


WATANZANIA wametakiwa kuwa na matumizi sahihi ya Kompyuta, Televisheni na Simu ili kuepusha athari katika miili yao.

Akizungumza katika Kanisa la Tanzania Assembiles of God Amani Cathedral Centre kwa Mchungaji Benjamin Bukuku, Mwezeshaji Konya Alex amesema vifaa hivyo ni muhimu katika utendaji wa kazi hususani katika Ulimwengu huu wa digitali.
Konya amesema watanzania hawatakiwi kuviacha kuvitumia kutokana na ukweli kwamba vina umuhimu mkubwa sana katika maisha ya kila siku hivyo umakini katika kutumia utapunguza athari katika miili ya binadamu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...