Language

Thursday 7 March 2013

HABARI MUHIMU: ZIMBABWE ITAJISIMAMIA YENYEWE KATIKA UCHAGUZI


Serikali ya Zimbabwe haitaruhusu wasimamizi wa nchi za Magharibi kuja kusimia kura ya maoni ya katiba mpya wiki ijayo na uchaguzi mkuu utakaofanyika katikati ya mwaka huu.
Serikali ya Rais Robert Mugabe imesemakuwa haitaruhusu wasimamizi kutoka mataifa ya Magharibi kuja nchini Zimbabwe kusimia zoezi la utoaji maoni kuhusu katiba mpya ya nchi hiyo wiki ijayo. Sambamba na hayo pia iserikali hiyo imedai hakutakuwa na haja ya kuja wasimamizi hao katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika katikati ya mwaka huu.

Waziri wa mambo ya nje wa Zimbambwe Simbarashe Mumbengwi ameiambia DW kuwa Umoja wa Ulaya pamoja nchi nyingine za Magharibi hawataruhusiwa kuingia nchini Zimbabwe kwa ajili ya kusimamia utoaji wa maoni unatarajiwa kufanyika juma lijalo na kwenye uchaguzi utakaofanyika katikati ya mwaka huu. Amesama wasimamizi kutoka mataiafa ya Afrika tu ndio watakaoalikwa kusimamimi zoezi hilo la Maoni ya katiba na uchaguzi uajao.
''Ispokuwa zile nchi ambazo sio adui wa Zimbabwe zitakaribishwa hapa, ama nchi ambapo zimehusika katika kuiwekea Zimbabwe vikwazo vya aina yoyote ,hazitakuwa na ruhusa ya kuja kwenye uchaguzi na zoezi la kutoa maoni kuhusu katiba ya Zimbabwe'' amsema wazei wa mambo yanje wa Zimbabwe
Mapema mwaka 2002 nchi za Maghari ikiwemo Marekani na Umoja wa uala EU zilimuekea vikwazo vya kiuchumi Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe pamoja na ofisa mkuu wa chama chake cha Zanu P-F.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...