Language

Thursday 17 January 2013

HABARI: WANAJESHI 200 WA NIGERIA KWENDA KUONGEZA NGUVU MALI

Takriban wanajeshi 200 wa Nigeria wanatarajiwa kuwasili nchini Mali kusaidia katika harakati dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu Kaskazini mwa nchi.

 

Ni kikosi cha kwanza cha jeshi kutoka Magharibi mwa Afrika kujiunga na wanajeshi wa Ufaransa walioanza kupambana na wapiganaji wa kiisilamu tangu Ijumaa iliyopita.
Wakati huohuo, wanajeshi wa Mali na Ufaransa, wameanza operesheni yao ya ardhini dhidi ya wapiganaji hao wa kiisilamu.
Duru zinasema kuwa makabiliano yalizuka kati ya waasi na wanajeshi mjini Diabaly, umbali wa kilomita 350 kaskazini mwa mji mkuu Bamako siku ya Jumatano.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...