Language

Thursday 17 January 2013

MICHEZO: PEP GUARDIOLA AMWAGA WINO BAYERN MUNICH MIAKA 3



Pep Guardiola, mwenye umri wa miaka 41, awali ilidhaniwa angelijiunga na Chelsea, au Manchester City, zote za Uingereza.


Guardiola ametia saini mkataba wa miaka mitatu na Bayern Munich, hadi mwaka 2016.
Atachukua madaraka ya Jupp Heynckes, ambaye ameamua kustaafu.
Siku zake akiwa mchezaji, Guardiola, aliwahi kuvichezea vilabu vya Barcelona, Brescia, Roma, Al.-Ahli, Dorados na pia timu ya taifa ya Uhispania.
Alikabidhiwa pia tuzo nyingi akiwa mchezaji.
Katika kazi ya meneja, amewahi kuchukua ubingwa wa ligi kuu ya Uhispania, La Liga, mara tatu, ushindi wa Supercopa de Espana mara tatu, mara mbili kutwaa ubingwa wa Copa Del Rey, ubingwa mara mbili wa klabu bingwa barani Ulaya, mara mbili Kombe la Uefa na vile vile mara mbili ubingwa wa Kombe la Dunia la FIFA kwa upande wa vilabu.
Guardiola, ambaye alizaliwa tarehe 18 Januari, mwaka 1971, Santpedor, Uhispania, tangu kuondoka uwanja wa Nou Camp mwezi Mei mwaka 2012, amepumzika msimu mzima, baada ya kukiwezesha klabu kupata jumla ya vikombe 14, ikiwa ni pamoja na ushindi wa klabu bingwa barani Ulaya mara mbili.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...