Language

Thursday 17 January 2013

MICHEZO: SUAREZ AKIRI KUJIANGUSHA KATIKA MEHI DHIDI YA STOKE CITY


 Luis Suarez

Msambulizi wa liverpool, Luis Suarez, ana amini kuwa analengwa sana na vyombo vya habari vya Uingereza lakini amekiri alijiangusha katika mechi moja ya ligi kuu msimu huu.

Katika mahojiana na kituo kimoja cha habari cha ametika ya kusini, mshambulizi huyo kutoka Uruguay, amesema kila mara yeye huangaziwa pakubwa na mashirika hayo kwa kuwa jina lake linafanya magazeti kuuza zaidi.
Suarez ambaye ndiye mfungaji bora wa liverpool msimu huu huku akiwa amefunga magoli 15, mawili nyuma ya nyota wa manchester United Robin van Persie, amekiri alijiangusha wakati wa mechi yao na Stoke City tarehe saba October mwaka uliopita.
Tangazo hilo la suarez limemuudhi kocha wa liverpool brendan roggers, ambaye amesema, mchezaji huyo ataadhibiw kuambatana na sheria za klabu hiyo.
Roggers, ametaja tangazo hilo la Suarez, kama moja ambalo kamwe halikubaliki.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...