Language

Saturday 16 March 2013

HABARI MUHIMU: HIVI UNAJUA KUWA PAPA FRANCIS I ALIKUWA BAUNSA WA MLANGONI BAA? SOMA HAPA UYAJUE MAISHA YAKE

Papa Francis I aliteuliwa hivi karibuni kuliongoza kanisa hilo baada ya Papa Benedict XVI kutangaza kujiuzulu kwa sababu za kiafya.

Enzi ya ujana wake aliwahi kufanya kazi mbalimbali ikiwamo ya mlinzi wa mlangoni (baunsa) katika Bar, ili kujipatia fedha.
Papa Francis aliteuliwa hivi karibuni kuliongoza kanisa hilo baada ya Papa Benedict XVI kutangaza kujiuzulu kwa sababu za kiafya.

Aidha, Papa Francis anatarajia kuongoza misa yake ya kwanza kesho katika Kanisa la Mtakatifu Peter, mjini Vatican.
Katika wasifu wake ulioandikwa mwaka 2010 na Francesca Ambrogetti na Sergio Rubin wa Shirika la Jesuit, Papa Francis I alikiri kuwa aliwahi kufanya kazi kama mlinzi wa mlangoni katika moja ya baa za Jimbo la Buenos, Argentina, ili kujipatia ada ya shule.
Papa huyu mpya ambaye jina lake halisi ni Jorge Mario Bergoglio, alisema kuwa rafiki yake wa kike alikuwa ni miongoni mwa kundi la marafiki aliokuwa akicheza nao muziki wa tango.
“Lakini baada ya kubaini kuwa natakiwa kuenenda kiroho, nilisitisha urafiki,” alisema alipohojiwa.
Papa Francis I amezaliwa katika familia yenye maisha ya kawaida, ambapo baba yake alikuwa mfanyakazi wa shirika la reli na mama yake alikuwa mama wa nyumbani.
Vilevile kuna taarifa zinaeleza kuwa Papa Francis, aliwahi kumpenda msichana mmoja na kutaka kuoa kabla ya kuingia katika utumishi wa Mungu.
Mwanamke huyo Amalia Damonte alisema kuwa aliwahi kutaka kuolewa na Papa, lakini alikataa.
“Nampa hongera Papa Francis, lakini nilikataa ombi lake la kutaka kunioa,” alisema Damonte.
Alisema Bergoglio alionyesha nia ya kumwoa akiwa na miaka 12 na alikataa kwa sababu wazazi wake wasingekubali akiwa katika umri huo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...