Language

Monday 14 January 2013

BURUDANI: JOKATE 'KIDOTI' KUOLEWA MWAKA HUU?

Miss Temeke 2006/07, Jokate Mwegelo 'Kidoti' anadaiwa kuchumbiwa kwa siri nyumbani kwao, Songea mkoani Ruvuma alipokwenda kusherehekea Sikukuu ya Mwaka Mpya.
Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa staa huyo, Jokate alitimba Songea akiongozana na rafiki zake wawili pamoja na baadhi ya ndugu.
Chanzo hicho kilidai kuwa kilipochunguza amekwenda kufanya nini mkoani humo, ndipo ikabainika kuwa alikwenda kusherehekea Mwaka Mpya akiongozana na wazazi wake anaoishi nao Dar, lengo likiwa kukamilisha mambo ya mila kwani alikuwa ameposwa na mchumba ambaye hakutajwa.
Mtu huyo aliendelea kudai kuwa nyumbani kwa akina Jokate ambaye aliapa kuwa lazima mwaka huu aolewe, kulikuwa na wageni wengi ambao miongoni mwao ndiyo waliopeleka posa.
Baada ya habari hizi kutua mezani,mwandishi wetu aliongea na Jokate kwa njia ya simu ambaye alikiri kwenda kwao Songea lakini hakutaka kudadavua ishu ya kuchumbiwa.
“Mh! Watu ni wambeya jamani! Mimi nilienda kwetu na ninatarajia kufanya kitu kikubwa huko Songea mtakisikia ‘soon’,” alisema Jokate huku akicheka.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...