Language

Thursday 14 March 2013

HABARI MUHIMU: XI JINPING RAIS MPYA CHINA


Bunge la uteuzi nchini China limemteua kiongozi wa Chama cha Kikomunisti, Xi Jinping, kuwa rais hatua inayomuweka kwenye kilele cha madaraka ya taifa hilo linalokuwa kwa kasi kubwa ya kiuchumi duniani.

Xi Jinping aliinama kwa heshima juu ya jukwaa kuu katika Ukumbi Mkuu wa Watu wa China, kama linavyoitwa jengo la bunge la nchi hiyo, huku wajumbe wakimpigia makofi ya kumpongeza katika tukio hilo lililorushwa moja kwa moja na televisheni ya taifa.

Kati ya kura 2,961 zilizohisabiwa, ni kura moja tu iliyomkataa, huku wajumbe watatu wakiripotiwa kutokuhudhuria mkutano huo maalum wa uteuzi. Kwa hivyo, akiwa mgombea pekee wa nafasi hiyo, Xi amepitishwa kwa asilimia 99.7 ya kura.
Tayari Xi alishachukua nafasi ya ukuu wa chama cha Kikomunsti kutoka kwa Hu hapo mwezi Novemba, na kabla ya kura ya leo kupigwa, mikutano ya awali ya viongozi wa kisiasa wa baraza hilo ilishalipitisha na kulipendekeza jina lake.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...