Language

Tuesday, 23 April 2013

N.E.C.T.A WAMEPANDISHA KIWANGO CHA UFAULU KIDATO CHA NNE, ANGALIA MARKS MPYA ZITAKAZOTUMIKA SASA


HIVI NDIVYO BARCELONA ALIVYOPIGWA NA 4 NA BAYERN MUNICH, ANGALIA SUMMARY YA MECHI YOTE HAPA



RATIBA YA MECHI KUBWA ZA APRILI 23 KATIKA MASHINDANO MBALI MBALI DUNIANI


HABARI KUBWA ZA APRILI 22 NA 23 KWA UFUPI


Boston attack motive still unclear Monday, April 22, 2013 11:34:02 PM
The motive for the Boston Marathon bombing remains unclear, after prosecutors charged the surviving suspect in hospital.
Explosion at French embassy in Libya Tuesday, April 23, 2013 12:21:52 AM
A car bomb explodes outside the French embassy in the Libyan capital, Tripoli, wounding two guards and causing extensive damage, officials say.
Japan warns China on islands landing Tuesday, April 23, 2013 12:19:39 AM
Japan would respond with force if any attempt is made to land on disputed islands, PM Shinzo Abe warns, as eight Chinese ships sail in the area.

MAREKANI YASHINIKIZA MAZUNGUMZO YA AMANI MASHARIKI YA KATI

Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Marekani John Kerry yuko mjini Brussels ambako anatarajiwa kukutana na mkuu wa Halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya Jose Manuel Barosso, na Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Urusi Sergei Lavrov. 

Kerry mwishoni mwa wiki alifanya ziara katika Ukingo wa Magharibi katika juhudi za kushinikiza kuanzishwa tena mazungumzo ya amani kati ya Israel na Palestina. Bruce Amani ana mengi zaidi
Akiwa mjini Istanbul hapo jana Jumapili, waziri huyo wa Mambo ya Kigeni wa Marekani John Kerry alimtaka Waziri Mkuu wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan kuchelewesha ziara yake katika Ukanda wa Gaza mnamo Mei 16 baada ya kuitembelea Ikulu ya Marekani, kwa sababu itahujumu juhudi za kuimarisha mahusiano baina ya Uturuki na Israel.

Monday, 22 April 2013

VAN PERSIE NA USHINDI WA 20 WA MANCHESTER UNITED

Manchester United imetwaa rasmi ubingwa wa 20 wa taji la ligi kuu soka nchini England kwa ushindi wa mabao matatu ya aina yake dhidi ya Aston Villa,Mabao yaliyofungwa kwa ustadi mkubwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Uholanzi Robin Van Persie ambaye sasa atakuwa akiongoza safu ya wafungaji kwa kufikisha mabao 24 huku Luis Suarez akifuatia akiwa na mabao 23.
Van Persie alifunga mabao yote matatu ndani ya dakika 31 za kipindi cha kwanza katika mchezo uliofanyika kwenye uwanja wa Old Traford na kuwafanya United kufikisha pointi tofauti ya 16 na waliokuwa mabingwa watetezi majirani zao Manchester City,huku wakiwa na michezo minne kibindoni.
Mkongwe Ryan Giggs alianza kwa kumtengenezea nafasi ya goli la kwanza Van Persie dakika mbili baada ya mchezo kuanza kabla ya Wayne Rooney kumpa nafasi nyingine nzuri Van Persie dakika ya 13 na kufunga moja kati ya mabao bora kabisa msimu huu kwa mguu wake wa kushoto na kufanya United kuwa mbele kwa mabao mawili ndani ya dakika 15 za kwanza za mchezo.

MANCHESTER UNITED KUTANGAZA UBINGWA LEO IWAPO ITASHINDA LEO DHIDI ASTON VILLA


Ligi kuu ya soka nchini England itaendelea tena jumatatu ya leo kwa mchezo mmoja kati ya Manchester United watakaokuwa nyumbani kwenye uwanja wa Old Traford kuwakaribisha Aston Villa.

Mchezo huo ambao Manchester United inahitaji ipate ushindi kujihakikisha ubingwa wa 20 wa ligi kuu soka nchini England na kuweka rekodi mpya ya kuwa timu iliyochukua taji hilo mara nyingi zaidi ya Liverpool ambayo ilikuwa inashikilia rekodi ya mataji 19.
United inakwenda kwenye mchezo huo ikiwa imetoka kulazimishwa sare ya 2-2 na West Ham United katika mchezo wa jumatano iliyopita. Aston Villa wao watashuka uwanjani kucheza mchezo huo usiku wa leo wakiwa kwenye harakati za kuepuka kushuka daraja la ligi kuu.
United katika michezo mitano iliyopita waliyocheza wamefungwa michezo miwili,wameshinda miwili na kutoka sare mmoja huku Aston Villa katika michezo mitano iliyopita waliyocheza wamefungwa mchezo mmoja na kushinda michezo mitatu na kutoka sare moja dhidi ya Fulham.
Huu utakuwa mchezo wa 34 kwa timu zote kwenye ligi kuu soka nchini Uingereza msimu huu ambapo zitakuwa zimebakisha michezo mingine minne kumaliza ligi.
United wanaongoza ligi wakiwa na point 81 huku wakifuatiwa na watani zao wa wajadi Manchester City ambao walifungwa hapo jana jumapili na Tottenham kwa mabao 3-1,hivyo mchezo wa leo utaweza kuwafanya United wacheze kwa uhuru zaidi na kutaka kujipa matumaini ya kuwavua rasmi ubingwa majirani zao Manchester City. Aston Villa inayofundishwa na Paul Lambert inashika nafasi ya 17 wakiwa na point 34,pointi tatu zaidi ya Wigan wenye pointi 31 wakiwa kwenye nafasi ya 18 ambayo ni kwenye kundi la timu tatu za mwisho zilizoko kwenye hatihati ya kushuka daraja.
Aston Villa katika michezo 32 iliyopita waliyocheza na Manchester United wameshinda mchezo mmoja,hiyo ilikuwa mwaka 2009 mwezi disemba pale Gabby Agbonlahor alipofunga bao la kichwa kwenye uwanja wa Old Traford. Kwa upande wa United, wao katika michezo 34 iliyopita ya ligi kuu tangu mwaka 1995 wamepoteza mara moja tu dhidi ya Villa.
Wayne Rooney anatarajia kufikisha mchezo wake wa 400 akiwa na Manchester United huku akiwa ameifungia klabu yake mabao tisa ya ligi kuu dhidi ya Aston Villa ikiwa ni rekodi nzuri kwake kuifunga timu moja idadi kubwa ya magoli,akiwa amezifunga idadi hiyo hivyo timu za Bolton, Fulham and Newcastle.

Sunday, 21 April 2013

WATU 185 WAPOTEZA MAISHA KATIKA MAPIGANO YA VIKUNDI VYA KIISLAMU NIGERIA


Mapigano ya wapiganaji wa kiislamu na vikosi vya usalama nchini Nigeria yameripotiwa kutokea tangu usiku wa Ijumaa na kuendelea kwa muda mrefu ambapo jumla ya watu 185 wanaripotiwa kufariki dunia katika mapigano hayo yaliyotokea Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Serikali ya mji wa Baga na Ofisa Serikali hiyo Bwana Lawan Kole.
Inasemekana kuwa watu wengi zaidi wamefariki dunia ambapo bado juhudi za kutafuta maiti nyingine zinaendelea. Brigedia Jenarali Austin Edokpaye amewaambia maafisa wakuu wa serikali kuwa,wapiganaji walitumia silaha kali na maroketi yenye mabomu mazito kupambana na vikosi vya jeshi.
Aidha bwana Edokpaye aliongeza kuwa,wapiganaji hao walikuwa wakitumia raia kama kinga yao kwa kujibanza karibu na makazi ya watu ambapo walijua vikosi vya jeshi visingeweza kujibu mapigo.

EXCLUSIVE!!! JUSTIN BIEBER NA SELENA GOMEZ WARUDIANA


Iliwahi kutokea mara ya kwanza Justin Bieber alipokuwa backstage katika moja ya matamasha yake, pia Justin na Selena Gomez wamekutwa wakibusiana (kiss) nyuma ya jukwaa katika shoo aliyofanya Justin mwishoni mwa wiki hii huko Norway.

Shuhuda wa tukio hilo amesema kuwa: “walikuwa wameshikana mikono muda wote, wakikumbatiana mara kwa mara na walikiss midomoni."
Kisha akaendelea"Wanaonekana wako penzini tena katika dimbwi zito la mapenzi, kana kwamba hawajawahi kugombana awali. Wanaonekana kabisa wamerudiana pamoja."
Justin na Selena walivunja uhusiano wao mwishoni mwa  mwaka 2012, lakini wote wawili walithibitisha kuwa bado wanawasiliana vizuri.
Kuna baadhi ya watu wao wa karibu waliwahi kusema kuwa  Gomez alikuwa akimtumia Bieber za kumuumiza pamoja na kumpigia simu na kumkumbushia mambo mengi ya kimapenzi waliyoenjoy pamoja kabla ya kutengana

Saturday, 20 April 2013

MAANDALIZI YA MADRID MARATHON YAMEPAMBA MOTO HISPANIA


Watu wengi zaidi wamejiandikisha kushiriki kwenye marathon ya Madrid, Uspania, ya Jumapili ya mwisho wa Aprili baada ya shambulio la bomu kwenye marathon ya Boston siku ya Jumatatu.

Waandalizi wa mbio hizo wanasema watu waliojiandikisha ilizidi mara nne baada ya shambulio la Boston.
Mkuu wa kamati ya Olimpiki ya Uspania ambayo inajitayarisha kuomba kuandaa Olimpiki ya mwaka wa 2020, alisema wanaoshiriki kwenye marathon wakiongezeka ndio sifa kubwa ambayo watu wa Madrid wanaweza kuupa mji wa Boston.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...