Language

Thursday, 25 April 2013

MATOKEO YA MECHI ZILIZOCHEZWA APRILI 25


UNAMFAHAMU ALIYEBUNI JINA LA TANZANIA? MSOME HAPA


HISTORIA ya Tanzania haiwezi kukamilika bila kutaja jina la mtu maarufu aliyebuni jina la Tanzania ambaye kwa bahati mbaya au kwa makusudi hakumbukwi tena.


Tunaelezwa kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, lakini nani kati yetu amekuwa akijiuliza jina la Tanzania lilivyopatikana na nani hasa alilibuni?
Wengi tunaambiwa kuwa jina la Tanzania lilipendekezwa na Watanganyika, Wazanzibari na raia wengine wa nje lakini hawatajwi waziwazi na picha zao tukaziona.
Inaaminika kuwa mtu aliyebuni jina la Tanzania ni MOHAMMED IQBAL DAR, raia wa India ambaye alikuwa miongoni mwa watu walioshindana katika shindano la kubuni jina la nchi mpya baada ya Tanganyika na Zanzibar kuungana.
Mohammed alizaliwa mkoani Tanga miaka ya 1944; baba mzazi wa Mohammed alikuwa daktari huko mkoani Morogoro akiitwa Dk. T . A DAR aliyefika Tanganyika kuanzia mwaka 1930.
Mohammed Iqbal Dar alipata elimu yake ya msingi mkoani Morogoro katika Shule ya Msingi H. H D Agakhan ambayo kwa sasa ni mali ya serikali. Alijiunga na Shule ya Sekondari Mzumbe alikosoma kidato cha kwanza hadi cha sita.

BRAZIL KUONGEZA NGUVU KATIKA KIKOSI DRC

Umoja wa Mataifa umemteua Generali mmoja raia wa Brazil ambaye anasifika kwa kudhibiti mtaa mmoja wa mabanda nchini Haiti kutokanamana na vurugu kuweza kuwaongoza walinda amani wa Umoja wa Mataifa katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Generali Carlos Alberto dos Santos Cruz ataongoza kikosi cha wanajeshi 20,000, ikiwemo kikosi kipya cha wanajeshi kitakachopambana na waasi mashariki mwa nchi.
Hii ndio mara ya kwanza kwa Umoja wa mataifa kukabidhi kikosi cha wanajeshi nguvu kuweza kupambana na waasi.
Generali Santos Cruz, aliambia BBC kuwa wanajeshi wake, watafunzwa namna watakavyo pambana na waasi bila kuwajeruhi raia na kuharibu mali nchini Congo.
"eneo tete zaidi siku hizi ni Mashariki mwa nchi,'' Cruz alimbia BBC
"niko tayari kukabiliana, na hali ngumu zaidi. Lengo kuu ni kuwaondolea hali ngumu wanayokabiliana nayo watu wa Congo.''

KURA ZA MAONI KUPIGWA JUU YA AMANI NCHINI MALI


Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kupigia kura azimio linalopendekeza kuundwa kwa kikosi cha kulinda amani nchini Mali.

Kikosi hicho chenye wanajeshi 12,600 kinajumuisha takriban wanajeshi 6,000 kutoka nchi za Magharibi mwa Afrika ambazo tayari zina wanajeshi wao nchini humo.
Azimio hilo limependekezwa na Ufaransa ambayo iliingilia kati mzozo wa Mali mnamo mwezi Januari ili kupambana na wapiganaji wa kiisilamu Kaskazini mwa nchi hiyo.
Kikosi hicho kinatarajiwa kwenda Mali mwanzoni mwa mwezi Julai kabla ya uchaguzi mkuu.

Wednesday, 24 April 2013

30 WAFARIKI KATIKA JENGO LA GHOROFA 8 KUPOROMOKA BANGLADESH

Vikosi vya uokoaji vinasema, watu wapatao 30 wamefariki dunia na mamia wengine wanahofiwa kukwama baada ya jingo la ghorofa nane kuporomoka katika mji mkuu wa Bangladesh, Dhaka.
Juhudi za ziada zinaendelea kuwaokoa watu walionaswa kwenye kifusi. Watu wapatao 200 wamejeruhiwa kufuatia ajali hiyo. Jeshi linasaidia shughuli za uokoaji katika eneo la tukio nje kidogo ya jiji la Dhaka.
Matukio ya majengo kuporomoka nchini Bangladesh ni ya kawaida kutokana na majengo mengi marefu kujengwa kinyume na sheria za ujenzi.
Jengo lililoporomoka lilikuwa na kiwanda cha nguo, benki na maduka kadhaa. Liliporomoka asubuhi wakati watu wakielekea makazini.
Watu wengi wamekusanyika karibu na eneo la tukio wakiwatafuta ndugu na marafiki. Mwandishi wa BBC mjini Dhaka anasema haijafahamika kilichosababisha jengo hilo kuporomoka, lakini vyombo vya habari nchini humo vimearifu kwamba, nyufa zilionekana kwenye jengo hilo siku ya Jumanne.

KILICHOANDIKWA NA MOJA PAGE YA FACEBOOK KUHUSIANA NA KUOKOKA KWA MWANAMUZIKI SIZE 8



KAMA HUKUZIPITA HABARI KUBWA ZA APRILI 24, ZOTE ZIKO HAPA


CIA 'tracked Boston bomb suspect' Wednesday, April 24, 2013 8:56:32 PM
The CIA added one of the Boston bomb suspects to a terrorism database 18 months ago, officials say, days after the FBI said it had also investigated him.
Frantic search for Dhaka survivors Wednesday, April 24, 2013 9:53:24 PM
Bangladeshi rescuers are desperately searching for survivors after a building housing garment factories collapsed in Dhaka, killing at least 147.
Two investigated over Kate images Wednesday, April 24, 2013 5:56:55 PM
Two people are under formal investigation in France over the publication of pictures of a sunbathing Duchess of Cambridge taken last autumn.
Teachers on rampage in Mexican state Wednesday, April 24, 2013 6:37:07 PM
Teachers incensed by sweeping education reforms are joined by vigilantes as they go on the rampage in Mexico, setting fires and vandalising offices.
Thumb-type keyboard takes on Qwerty Wednesday, April 24, 2013 7:03:06 PM
Researchers create a keyboard which they claim allows people to "thumb-type" faster on touchscreen devices.
S Korea proposes factory zone talks Wednesday, April 24, 2013 8:43:26 PM
South Korea proposes formal talks with the North over the jointly-run Kaesong industrial park, warning of "grave measures" if the offer is rejected.
Ancient Aleppo minaret destroyed Wednesday, April 24, 2013 8:34:22 AM
The minaret of Syria's famous 12th-Century Umayyad Mosque in the northern city of Aleppo is destroyed as rebels clash with government troops.
Capriles issues vote 'ultimatum' Wednesday, April 24, 2013 9:13:26 PM
Venezuelan opposition candidate Henrique Capriles threatens unspecified action unless details are released of an audit of 14 April presidential polls.
Facebook 'must remove memorial page' Wednesday, April 24, 2013 3:03:34 PM
A court in Brazil has backed a mother's plea to have the Facebook profile of her deceased daughter taken offline.
Argentine activists lobby Pope Wednesday, April 24, 2013 4:09:24 PM
Argentine activists campaigning for information on children stolen during the Dirty War ask the Pope to open Vatican archives from the period.


MATOKEO YA MECHI KUBWA ZA APRILI 24


HIVI NDIVYO LEWANDOWSKI ALIVYO WAFUNGA REAL MADRID GOLI 4



UBAROZI WA UFARANSA LIBYA WALIPULIWA


Bomu limelipuka nje ya ubalozi wa Ufaransa katika mji mkuu wa Libya, Tripoli na kuwajeruhi walinzi wawili huku ikisababisha uharibifu mkubwa. 

Mlipuko huo ulisababisha uharibifu katika sehemu moja ya ofisi hizo na pia kuharibu nyumba jirani.
Mwandishi wa BBC mjini Tripoli, Rana Jawad anasema kuwa inaaminika kuwa mlipuko huo ulisababishwa na gari lililokuwa na mabomu.
Rais wa Ufaransa, Francois Hollande, aliitaka serikali ya Libya kuchukua hatua za haraka kukabiliana na waliosababisha shambulio hilo.
Aliongeza kwamba shambulizi hilo lililenga nchi za kigeni zinazopambana dhidi ya ugaidi.
Balozi za kigeni nchini Libya zimewahi kushambuliwa katika siku za nyuma, lakini hili ndilo shambulizi la kwanza kubwa dhidi ya ubalozi wa kigeni mjini Tripoli.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...