Language

Friday 8 March 2013

HABARI MUHIMU: BABA MKWE WA OSAMA BIN LADEN KUFIKISHWA MAHAKAMANI MAREKANI


Mkwe wa kiume wa Osama bin Laden anatarajiwa kufika mbele ya mahakama moja mjini New York Marekani leo Ijumaa kwa mashtaka ya kupanga njama ya kuwauwa Wamarekani.

Sulemain Abu Ghaith ambaye ni mwanamgambo aliyeonekana katika mikanda ya video akiwakilisha mtandao wa kigaidi wa Al Qaeda baada ya mashambulio Septemba mwaka 2001,alikamatwa nchini Uturuki wiki iliyopita na kusafirishwa hadi Marekani kushitakiwa.

Abu Ghaith aliyezaliwa Kuwait amekuwa msemaji wa mtandao huo wa kigaidi na alikuwa mshirika wa karibu sana wa baba mkwe wake,Osama. Amekuwa akisifia sana mashambulio ya kigaidi ya septemba 11 mwaka 2001 na kuonya kuwa kutakuwa na mashambulio hata zaidi.
Kesi dhidi yake ni ushindi mkubwa kisheria kwa utawala wa Rais Barrack Obama ambao umekuwa ukitafuta kwa muda mrefu kuwashtaki washukiwa wakuu wanaohusishwa na Al Qaeda badala ya kuwazuia tu katika kambi ya kijeshi ya Guantanamo Bay iliyoko Cuba. Kuwashtaki washukiwa wakuu wa kigaidi katika mahakama za Marekani ilikuwa mojawapo ya ahadi kuu alizotoa Rais Obama punde tu baada ya kuchukua madaraka mwaka 2009 akilenga kufunga kambi hiyo ya Guantanamo Bay.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...