Language

Friday 8 March 2013

MICHEZO: SIMBA YAMKABIDHI MALKIA WA NYUKI MADARAKA

Baada ya siku moja kupita kufuatia viongozi wawili wa kamati ya utendaji ya Simba kutangaza kujiuzulu, mwenyekiti wa baraza la wadhamini la klabu ya Simba mzee Joseph Itangile maarufu kama mzee Kinesi hii leo ametangaza mabadiliko ya dharura ya  uongozi wa klabu ya klabu hiyo.

Katika mabadiliko hayo mzee Kinesi amesema kuanzia hii jana nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Hans Poppe aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu hiyo sasa itakuwa ikishikiliwa na Bi Rahma Al Harouz( malkia wa nyuki) huku nafasi ya makamu mwenyekiti wa klabu hiyo iliyokuwa ikishikiliwa na Geoffrey Nyange Kaburu sasa itakuwa ikikaimiwa na yeye mwenyewe.
Mabadiko hayo yamefuatia kikao cha dharura cha wajumbe wa kamati ya utendaji ya Simba kilicho fanyika jana usiku bila ya kuwepo mwenyekiti Alhaji Ismail Aden Rage ambaye yuko nchini India akifanyiwa matibabu ambaye hata hivyo baada ya mawasiliano kufanyika alikubali na kubariki mabadiliko hayo.
Mzee Kinesi amesema kwamba kwasasa klabu ya Simba bado ina umoja na katika kipindi hiki wameunda kamati ya ushindi ambayo itakuwa chini ya Malkia wa nyuki na kwamba ni wakati wa kuondoa mipasuko ndani ya klabu hiyo.
Jioni hii uongozi wa klabu ya Simba umetembelea tawi la mpira pesa kwa lengo la kuvunja mpasuko ndani ya klabu hiyo na kujenga umoja.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...