Language

Saturday 13 April 2013

AFRICAN LYON NA HOMA YA KUSHUKA DARAJA



Kocha wa African Lyon, Charles Otieno amesema kwa sasa wanaomba Toto African, Polisi Morogoro wapoteze michezo yao ili wasalimike na janga la kushuka daraja.
 
Kocha huyo alikiri hawana njia mbadala ya kukwepa janga la kushuka daraja kama si kuomba dua mbaya kwa Toto na Polisi tu kwa sasa.
“Siwezi kusema tumeshuka, bado tunamichezo mitatu mkononi endapo tutashinda uwezekano ni mkubwa wa kuendelea kubaki, hakuna njia ya kutubakiza zaidi ya Polisi na Toto kupoteza mechi zao ili sisi tuweze kupata nafasi kinyume na hapo ni lazima tutashuka tu”alisisitiza kocha huyo.
Lyon imebakiza mechi dhidi ya JKT Ruvu, Mtibwa Sugar pamoja na Mgambo JKT. (Jessca Nangawe)Text inakuja hapa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...