Maoni mbalimbali yanaendelea kutolewa nchini Tanzania juu ya ripoti ya
mdhibiti mkuu na mkaguzi wa hesabu za serikali nchini humo, iliyomulika kiwango
kikubwa cha ubadhirifu wa fedha za umma katika serikali hiyo.
Ripoti hiyo imeaziangazia sekta au idara ya ujenzi, nishati na
madini kuwa miongoni mwa idara zinazokuwa na ubadirifu wa fedha za umma.
Hata hivyo swali linaloulizwa ni je tatizo liko wapi kiasi ya kuwapo
ubadhirifu mkubwa wa mara kwa mara katika fedha za umma? Amina Abubakar
amezungumza na Profesa Ibrahim Lipumba ni mtaalamu bingwa wa uchumi nchini
Tanzania.Kusiikiliza mazungumzo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.
No comments:
Post a Comment