Language

Friday 1 March 2013

BURUDANI: PREZZO AMEGOMA KUMUONGELEA GOLDIE


Tangu kurudi kwake Nigeria, na kutengwa kuhudhuria mazishi ya anayedaiwa kuwa mpenzi wake, Goldoe Harvey nyota wa Big Brother toka nchini Kenya, John Makini anayejulikana zaidi kwa jina la Prezzo hajasema lolote kwa vyombo vya habari kuhusiana na majanga yaliyompata huko.


Prezzo, alikuwa Nigeria ambako alikwenda kwa ajili ya Sikukuu ya Wapendanao na kukutana na kifo cha mshiriki mwenzake wa Big Brother na mwanamuziki Mnaijeria, Goldie Harvey ambaye inaaminika walikuwa na uhusiano wa kimapenzi.
Kilichokuja kuibuka na kumchanganya zaidi Prezzo ni mtu anayejulikana kwa jina la Andrew Harvey ambaye aliachia mtandaoni picha za harusi yake na mwanadada Goldie Harvey, ambaye pia siku chache zilizopita alionekana Nigeria akihudhuria mazishi ya mwanadada huyo.
Prezzo kwa upande wake, aliwaambia wanahabari kwamba anahitaji muda wa kupumzika kabla ya kusema lolote.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...