Language

Thursday 28 March 2013

TIMBULO: SKENDO HAZIJACHANGIA KUNIONGEZEA UMAARUFU


Msanii wa bongofleva Timbulo amesema kuwa yeye si msanii ambaye amepata umaarufu kutokana na skendo kuliko kazi anayofanya ya muziki.

Timbulo amesema kuwa watu wanaosema kuwa yeye anapendwa kutengeneza skendo ili aandikwe kwenye magazeti wanakosea kwa kuwa angetaka kufanya hivyo basi angekuwa anatengeneza stori nzuri na si za kumchafua.
Msanii huyo alisema kuwa hajawahi kufanya kitu kama hicho kabisa, "kuna vitu vya kutengeneza lakini si kashfa ambayo inaweza kuwa kidonda cha milele, ningekuwa nataka kutengeneza kashfa nzuri basi ni bora ningetengeneza stori za uwongo kuwa nimeenda kutoa msaaada sehemu flani lakini si kwa kujichafua jina langu".
Tangu atoke na wimbo wa kwanza 'Domo langu' mwaka 2011 msanii huyo amekuwa akiandikwa kwenye magazeti kwa skendo kuliko kazi anazofanya.

Hivi karibuni pia Timbulo aliwahi kuripotiwa kwamba amekamatwa na madawa ya kulevya nchini burundi huku picha yake akiwa na madawa ikisambazwa kwenye mitandao mbali mbali ya kijamii na magazeti tando,n lakini siku chache baadae, tukio hilo lilikanushwa.
Timbulo ambaye jina lake halisi ni Ally Timbulo aliongeza pia kuwa alikuwa atoe wimbo wake wiki hii kabla ya Pasaka lakini kutokana na yeye kupata onyesho la pasaka mkoani atashindwa kutoa wimbo wake mpya.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...